Anasema Mwenyezi Mungu Mtukufu: Hana mja wangu muumini toka kwangu malipo yoyote pindi ninapomchukua kipenzi chake katika familia yake duniani kisha akasubiri (malipo mazuri) zaidi ya pepo

Anasema Mwenyezi Mungu Mtukufu: Hana mja wangu muumini toka kwangu malipo yoyote pindi ninapomchukua kipenzi chake katika familia yake duniani kisha akasubiri (malipo mazuri) zaidi ya pepo

Kutoka kwa Abuu Huraira -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- Hadithi Marfu'u: "Anasema Mwenyezi Mungu Mtukufu: Hana mja wangu muumini toka kwangu malipo yoyote pindi ninapomchukua kipenzi chake katika familia yake duniani kisha akasubiri (malipo mazuri) zaidi ya pepo".

[Sahihi] [Imepokelewa na Al-Bukhaariy]

الشرح

Anaeleza Nabii -Ziwe juu yake Amani- katika hadithil Qudsiy hii, kuwa yeyote atakayetahiniwa kwa kumkosa kipenzi chake miongoni mwa ndugu wa karibu au yeyote, atakaposubiri mwanadamu juu ya kuondokewa na yule aliyemteua na kumchagua na akaona kua huyu ndiye mwenye mahusiano mazuri na yeye, kama mtoto, au baba mdogo, au baba, au mama, au rafiki, anapomchukua Mwenyezi Mungu Mtukufu kisha mwanadamu akataraji malipo basi hana malipo mengine zaidi ya pepo.

التصنيفات

Ubora na fadhila za matendo mema.