إعدادات العرض
Peaneni zawadi, mtapendana
Peaneni zawadi, mtapendana
Imepokelewa kutoka kwa Abuu Huraira -radhi za Allah ziwe juu yake- kutoka kwa Mtume -rehema na amani ziwe juu yake- anasema: "Peaneni zawadi, mtapendana."
[Ni nzuri (Hasan)] [Imepokelewa na Bukhari katika Al-Adab Al-Mufrad na Abuu Ya'laa na Al-Bayhaqiy]
الترجمة
العربية বাংলা دری Português Македонски ไทย Tiếng Việt Magyar ქართული Indonesia Kurdî Hausa Tagalog অসমীয়া മലയാളം English ગુજરાતી Nederlands ਪੰਜਾਬੀ ភាសាខ្មែរ සිංහල Русский मराठीالشرح
Mtume rehema na amani ziwe juu yake amemhimiza Muislamu kuwa abadilishane zawadi na ndugu yake Muislamu, na kuwa zawadi ni miongoni mwa sababu za mapenzi na kuziunganisha nyoyo.فوائد الحديث
Ni sunna kutoa zawadi; kwa sababu Mtume rehema na amani ziwe juu yake ameamrisha kufanya hivyo.
Zawadi ni sababu ya kuleta mapenzi.
Inampasa mwanadamu afanye kila ambacho ndani yake kinaleta mapenzi kati yake na watu wengine, sawa sawa iwe ni katika zawadi au kuwa mpole, au katika maneno mazuri au katika ukunjufu wa uso kwa kadiri awezavyo.
التصنيفات
Kutoa Bure na Utoaji wabadala.