Alitawadha Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- mara moja moja

Alitawadha Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- mara moja moja

Imepokewa kutoka kwa Bin Abbas -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yao- amesema: Alitawadha Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- mara moja moja.

[Sahihi] [Imepokelewa na Al-Bukhaariy]

الشرح

Alikuwa Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- katika baadhi ya nyakati zake anapotawadha anaosha kila kiungo katika viungo vya udhu mara moja moja, anaosha uso pamoja kusukutua na kupandisha maji puani, na mikono miwili na miguu miwili mara moja moja, na hiki ndicho kiwango cha wajibu.

فوائد الحديث

Kilicho wajibu katika kuosha viungo ni mara moja moja, inayozidi inapendeza kufanya hivyo.

Sheria ya kutia udhu mara moja moja katika baadhi ya nyakati.

Sheria katika kufuta kichwa ni mara moja.

التصنيفات

Sunna na Adabu za Kutawadha, Sifa za Kutawadha.