Tulikuwa pamoja Mtume rehema na amani ziwe juu yake nasi tukiwa vijana karibu na balehe, tukajifunza imani kabla ya kujifunza Qur'ani, kisha tukajifunza Qur'ani, tukaongeza imani kupitia Qur'ani

Tulikuwa pamoja Mtume rehema na amani ziwe juu yake nasi tukiwa vijana karibu na balehe, tukajifunza imani kabla ya kujifunza Qur'ani, kisha tukajifunza Qur'ani, tukaongeza imani kupitia Qur'ani

Imepokelewa kutoka kwa Jundubu bin Abdillah radhi za Allah ziwe juu yake amesema: Tulikuwa pamoja Mtume rehema na amani ziwe juu yake nasi tukiwa vijana karibu na balehe, tukajifunza imani kabla ya kujifunza Qur'ani, kisha tukajifunza Qur'ani, tukaongeza imani kupitia Qur'ani.

[Sahihi] [Imepokelewa na Ibnu Maajah]

الشرح

Amesema Jundubu bin Abdillah radhi za Allah ziwe juu yake: Tulikuwa pamoja na Mtume rehema na amani ziwe juu yake nasi tukiwa vijana tuliokaribia kubalehe, wenye nguvu na wakali, tukajifunza kwa Mtume rehema na amani ziwe juu yake imani kabla ya kujifunza Qur'ani, kisha tukajifunza Qur'ani; tukazidisha imani kupitia Qur'ani.

فوائد الحديث

Kumebainishwa kuwa imani inazidi na kupungua.

Kupangilia vipaumbele wakati wa kumlea kijana anaekua, na pupa ya kuwajaza imani.

Qur'ani huzidisha imani, na moyo hung'aa kupitia hiyo, na kifua hukunjuka.

التصنيفات

Adabu za Usomaji Qur;an na Ubebaji wa Qur'an., Kuzidi kwa Imani na Kupungua kwake.