إعدادات العرض
Akasema: Alikuwa akishiriki katika kazi za familia yake (anakusudia kuhudumia familia yake), unapofika wakati wa swala anatoka kwenda katika swala
Akasema: Alikuwa akishiriki katika kazi za familia yake (anakusudia kuhudumia familia yake), unapofika wakati wa swala anatoka kwenda katika swala
Kutoka kwa Aswadi bin Yadizi amesema: Nilimuuliza Aisha, nini alikuwa akifanya Mtume rehema na amani ziwe juu yake nyumbani kwake? Akasema: Alikuwa akishiriki katika kazi za familia yake (anakusudia kuhudumia familia yake), unapofika wakati wa swala anatoka kwenda katika swala.
[Sahihi] [Imepokelewa na Al-Bukhaariy]
الترجمة
العربية বাংলা Bosanski English Español فارسی Français Bahasa Indonesia Русский Tagalog Türkçe اردو 中文 हिन्दी සිංහල ئۇيغۇرچە Kurdî Tiếng Việt Magyar ქართული mr Română অসমীয়াالشرح
Aliulizwa mama wa Waumini Aisha radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake kuhusu hali ya Mtume rehema na amani ziwe juu yake nyumbani kwake, na alikuwa akifanya nini? Akasema: Alikuwa ni mtu kama watu wengine, na anafanya wanayofanya wanaume katika majumba yao, anashughulika na kujihudumia yeye na familia yake; anakamua mbuzi wake mwenyewe, na anashona nguo yake, na anashona kiatu chake, na anatengeneza ndoo yake, na ulikuwa unapofikia wakati wa kusimamishwa swala anatoka kwa ajili yakusali rehema na amani ziwe juu yake bila kuchelewa.فوائد الحديث
Ukamilifu wa unyenyekevu wake rehema na amani ziwe juu yake na wema wake kwa familia yake.
Amali za kidunia hazitakiwi kumshughulisha mja akawacha swala.
Kuhifadhi kwake Mtume rehema na amani ziwe juu yake swala, mwanzo wa wakati wake.
Amesema bin Hajari: Na hapa kunahimizo la kuwa mnyenyekevu na kuacha kiburi na mwanaume kuihudumia familia yake.