Yakuwa aliulizwa kuhusu kisomo cha Mtume rehema na amani ziwe juu yake

Yakuwa aliulizwa kuhusu kisomo cha Mtume rehema na amani ziwe juu yake

Kutoka kwa Abuu Mulaika: Kutoka kwa baadhi ya wake za Mtume rehema na amani ziwe juu yake, amesema: Abuu Aamir, amesema Naafii: Nafikiri ni Hafswa -Yakuwa aliulizwa kuhusu kisomo cha Mtume rehema na amani ziwe juu yake akasema: Hakika nyinyi hamkiwezi, akasema: Akaambiwa hebu tueleze. Akasema: Akasoma kisomo cha taratibu, akasema Abuu Aamiri: Akasema Naafii: Akatusimulia Abuu Mulaika: "Alhamdulillaah Rabbil-Aalamiin" [Al-Faatiha: 1] Kisha akakata "Al Rahmaanir Rahiim" [Faatiha:3] kisha akakata "Maaliki yaumid diin".

[Sahihi] [Imepokelewa na Ahmad]

الشرح

Aliulizwa Hafswa mama wa waumini radhi za Allah ziwe juu yake: Kilikuwa vipi kisomo cha Qur'ani cha Mtume rehema na amani ziwe juu yake? Akasema: Hakika nyinyi hamkiwezi mfano wake, akaambiwa: Tueleze. Amesema Naafii: Akatusomea Abuu Mulaika kisomo alichotulizana ndani yake; ili kielezee na kikaribiane na kisomo cha Mtume rehema na amani ziwe juu yake, akasoma: "Alhamdulillaahi Rabbil Aalamiin" kisha akakata kisomo, "Al Rahmaanir Rahiim", kisha akakata kisomo, "Maaliki yaumid diin".

فوائد الحديث

Kumebainishwa muongozo wa Mtume rehema na amani ziwe juu yake katika kusoma Qur'ani.

Kufanya kwa vitendo ili kubainisha namna ya kisomo cha Mtume rehema na amani ziwe juu yake.

Sheria ya kwenda taratibu katika kuisoma Qur'ani, hilo huleta msukumo wa kuizingatia.

Kuitilia maanani Qur'ani wema waliotangulia, na matendo ya Mtume rehema na amani ziwe juu yake.

Umuhimu wa kujua kanuni za kuisoma Qur'ani (Tajwidi) na elimu za Qur'ani.

التصنيفات

Elimu ya Tajwiid.