Hakika ndani ya Pepo kuna mti ambao anatembea aliyepanda kipando madhubuti chenye uimara na kasi kubwa ya kukimbia kwa muda wa miaka mia moja na haumalizi (kuuvuka) mti huo

Hakika ndani ya Pepo kuna mti ambao anatembea aliyepanda kipando madhubuti chenye uimara na kasi kubwa ya kukimbia kwa muda wa miaka mia moja na haumalizi (kuuvuka) mti huo

Imepokelewa kutoka kwa Abii Saidi Al-Khudry radhi za Allah ziwe juu yake kutoka kwa Mtume rehema na amani ziwe juu yake amesema: "Hakika ndani ya Pepo kuna mti ambao anatembea aliyepanda kipando madhubuti chenye uimara na kasi kubwa ya kukimbia kwa muda wa miaka mia moja na haumalizi (kuuvuka) mti huo".

[Sahihi] [Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim]

الشرح

Ameeleza Mtume rehema na amani ziwe juu yake ya kwamba peponi kuna mti ambao anatembea chini yake aliyepanda Farasi aliyeandaliwa kwa mashindano, na mwenda kasi zaidi katika kukimbia kwake miaka mia moja lakini hafiki mwisho wa yanakolalia matawi yake.

فوائد الحديث

Hapa kumebainishwa upana wa Pepo, na ukubwa wa miti yake.

التصنيفات

Sifa za pepo na moto.