إعدادات العرض
Alikuwa Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- akifanya juhudi katika ramadhani kwa namna ambayo hajitahidi katika nyakati zingine nje ya ramadhani, na katika kumi la mwisho pia alikuwa na juhudi ambazo hakuwa anajitahidi hivyo nje ya ramadhani
Alikuwa Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- akifanya juhudi katika ramadhani kwa namna ambayo hajitahidi katika nyakati zingine nje ya ramadhani, na katika kumi la mwisho pia alikuwa na juhudi ambazo hakuwa anajitahidi hivyo nje ya ramadhani
Kutoka kwa Aisha -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- Amesema: Alikuwa Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- akifanya juhudi katika ramadhani kwa namna ambayo hajitahidi katika nyakati zingine nje ya ramadhani, na katika kumi la mwisho pia alikuwa na juhudi ambazo hakuwa anajitahidi hivyo nje ya ramadhani.
[Sahihi] [Imepokelewa na Imamu Muslim]
الترجمة
عربي বাংলা Bosanski English Español فارسی Français Bahasa Indonesia Русский Tagalog Türkçe اردو 中文 हिन्दी Hausa Kurdî Português සිංහලالشرح
Anaeleza Aisha -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- katika hadithi, kuhusu ibada zake -Rehema na Amani ziwe juu yake- katika mwezi wa ramadhani, nayo nikuwa yeye alikuwa akijitahidi ndani yake kwa kiasi ambacho hajitahidi katika miezi isiyokuwa ramadhani; hakika huo ni mwezi wenye baraka, ameufanya bora Mwenyezi Mungu kuliko miezi mingine, zinapoingia siku kumi za mwisho anajitahidi ndani yake zaidi kuliko jinsi alivyokuwa mwanzo wa mwezi; kwasababu ndani yake kuna usiku wa cheo (Lailatul Qadri) ambao ni bora kuliko miezi elfu moja, na kwasababu siku hizo ndizo za mwisho wa mwezi wenye baraka, akawa anauhitimisha kwa matendo mema.