Neema mbili wamepoteza thamani yake watu wengi: Afya na wakati

Neema mbili wamepoteza thamani yake watu wengi: Afya na wakati

Imepokelewa kutoka kwa bin Abbas -radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- amesema: Amesema Mtume wa Mwenyezi Mungu -rehema na amani ziwe juu yake-: "Neema mbili wamepoteza thamani yake watu wengi: Afya na wakati".

[Sahihi] [Imepokelewa na Al-Bukhaariy]

الشرح

Alieleza Mtume rehema na amani ziwe juu yake kuhusu neema mbili kubwa miongoni mwa neema za Mwenyezi Mungu kuwa wanapata hasara ndani yake watu wengi, kiasi kwamba wanazitumia mahali pasipostahiki; kwani mwanadamu zikikusanyika kwake neema ya afya na wakati, akazidiwa na uvivu wa kufanya ibada basi kapata hasara; na ndio hali ya watu wengi, na akiutumia muda wake na afya yake katika kumtii Mwenyezi Mungu basi atakuwa kapata faida; hii ni kwa sababu dunia ndio shamba la Akhera, na wakati hufuatiwa na shughuli, na afya hufuatiwa na maradhi, na lau kusingekuwa na chochote zaidi ya uzee basi ungetosha.

فوائد الحديث

Kumfananisha mtu mzima na mfanya biashara, na afya na muda kavifananisha na mtaji; atakayeutumia vizuri mtaji wake atapata faida, na atakayeupoteza basi atapata hasara na kujuta.

Amesema bin Khaazin: Neema ni kila anachoneemeka nacho mtu na anapata ladha kwacho, na udanganyifu, ni mtu kununua kitu kwa thamani kubwa, au kukiuza kwa thamani isiyolingana na kilichouzwa; atakayekuwa na afya katika mwili wake na akawa na wakati na hana la kumshughulisha, na akawa hakwenda mbio kuitumikia Akhera yake huyu ni sawa na aliyefanya biashara yenye udanganyifu.

Kuwa na pupa ya kufaidika na afya na wakati kwa ajili ya kujikurubisha kwa Mwenyezi Mungu Aliyetakasika na Kutukuka, na kufanya kheri kabla ya kutoweka kwake.

Kushukuru neema za Mwenyezi Mungu kunakuwa kwa kuzitumia katika kumtii Mwenyezi Mungu Mtukufu.

Amesema Kadhi Abubakari bin Al-Arabi: Kumepatikana tofauti kuwa ni ipi neema ya kwanza kwa mja, kukasemwa: Ni imani, na kukasemwa: Ni uhai, na kukasemwa: Ni afya, na ya kwanza ndio bora kwa sababu ndio neema ya kiujumla, na ama uhai na afya hizo ni neema za kidunia, na wala haziwezi kuwa neema halisia isipokuwa zitakapoambatana na imani, na hapo ndipo wanapohadaika watu wetu, yaani inapotea faida yao au inapungua, atakayeiendekeza nafsi yake yenye kuamrisha maovu, na yenye kudumu katika starehe, akaacha kuhifadhi mipaka ya Mwenyezi Mungu, na kudumu na ibada, basi huyu atakuwa kahadaika, na vile vile atakapokuwa hana la kumshughulisha, kwa sababu aliyeshughulishwa anaweza kuwa na udhuru tofauti na mwenye nafasi; basi huyu hana udhuru na hoja itasimama juu yake.

التصنيفات

Kuzitakasa Nafsi.