Tahadharini sana na kuingia/kukaa kwa wanawake" Mtu mmoja katika Maanswari akasema: Ewe Mtume wa Allah vipi kuhusu shemeji? Akasema: "Shemeji ni kifo

Tahadharini sana na kuingia/kukaa kwa wanawake" Mtu mmoja katika Maanswari akasema: Ewe Mtume wa Allah vipi kuhusu shemeji? Akasema: "Shemeji ni kifo

Imepokelewa kutoka kwa Uqbah bin Aamir -radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- Yakwamba Mtume -rehema na amani ziwe juu yake: "Tahadharini sana na kuingia/kukaa kwa wanawake" Mtu mmoja katika Maanswari akasema: Ewe Mtume wa Allah vipi kuhusu shemeji? Akasema: "Shemeji ni kifo".

[Sahihi] [Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim]

الشرح

Ametahadharisha Mtume rehema na amani ziwe juu yake swala la kuchanganyikana na wanawake wa kando, na akasema: Jiepusheni sana kuingia kwa wanawake, na wanawake watahadhari kuingia kwa wanaume. Akasema mtu mmoja miongoni mwa Manswari (watu wa Madina): Wasemaje kuhusu ndugu wa karibu wa mume; kama kaka wa mume na mtoto wa kaka yake, na ami yake na mtoto wa ami yake, na kijana wa dada yake, na mfano wa hao katika wale wa halali kwao kumuoa akiwa hajaolewa? Akasema Mtume rehema na amani ziwe juu yake: Mtahadharini kama mnavyokitahadhari kifo! Kwa sababu kukaa faragha na mashemeji kunapelekea fitina na maangamivu katika dini, ndugu wa mume wasiokuwa baba zake na wanawe, hawa wanatakiwa zaidi kuzuiliwa kuliko hata mtu wa kando; kwa sababu kukaa faragha na ndugu wa mume ni zaidi ya kukaa faragha na mtu mwingine, na shari iko karibu zaidi kwake kutokea kuliko hata kwa asiyekuwa yeye, na kuna uwezekano mkubwa wa kutokea; kwa sababu anauwezekano mkubwa wa kumfikia mwanamke na kukaa naye faragha pasina mtu wa kuwakemea, na ni kwa sababu hana budi lazima aonane naye kwakuwa ni ndugu wa mume, na ni vigumu kumzuia, kwa sababu tamaduni za watu zimezoeleka kulipuuza hilo, mtu akakaa faragha na mke wa kaka yake; hivyo anafanana na kifo katika ubaya na madhara, tofauti na mwanaume wa kando kwani huyo watu humtahadhari.

فوائد الحديث

Katazo la kuingia kwa wanawake wa kando na kukaanao faragha, kwa ajili ya kuziba njia zinazopelekea kuingia katika uchafu.

Katazo hilo ni kwa watu wa kando wote kwanzia kaka wa mume na ndugu zake wa karibu, ambao si haramu kwao kumuoa mwanamke, hivyo ni lazima kuchunguza ili kujua kama kuingia kwake kunapelekea kuwa faragha.

Kujiweka mbali na maeneo yote ya kuteleza, kwa kuhofia kuingia katika shari.

Amesema Imam Nawawi: Wamekubaliana wasomi wote wa Lugha ya kiarabu kuwa maana ya mashemeji ni ndugu wa karibu wa mume, kama baba yake na ami yake, na kaka yake, na mtoto wa kaka yake, na mtoto wa ami yake na mfano wao, nakuwa wakwe ni ndugu wa karibu wa mume, nakuwa wakwe wanakuwa kwa aina zote mbili.

Ameufananisha ushemeji na kifo, amesema bin Hajari: Na waarabu hukifananisha kitu chenye kuchukiza na kifo, na namna ya kufanana kwake nikuwa ni kifo cha dini yakitokea maasi, na ni kifo cha mambo yote endapo yatatokea maasi kwani itakuwa wajibu kupigwa mawe, na ni kifo cha mwanamke kwa kuachana na mumewe endapo wivu utampelekea kumpa talaka.

التصنيفات

Hukumu za wanawake.