Ewe Abuu Dhari utakapopika mchuzi basi zidisha maji yake, na umkumbuke jirani yako

Ewe Abuu Dhari utakapopika mchuzi basi zidisha maji yake, na umkumbuke jirani yako

Kutoka kwa Abuu Huraira -radhi za Allah ziwe juu yake- amesema: Amesema Mtume -rehema na amani ziwe juu yake-: "Ewe Abuu Dhari utakapopika mchuzi basi zidisha maji yake, na umkumbuke jirani yako".

[Sahihi] [Imepokelewa na Imamu Muslim]

الشرح

Alimhimiza Mtume rehema na amani ziwe juu yake Abuu Dhari Al-Ghifaari radhi za Allah ziwe juu yake atakapopika mchuzi basi azidishe maji yake na mchuzi wake, na amkumbuke na amtafute jirani yake.

فوائد الحديث

Himizo la kuwa na mahusiano mazuri na jirani.

Sunna ya kupeana zawadi kati ya majirani wawili; kwa sababu hilo linaleta mapenzi na mahaba, na kunakuwa na mkazo zaidi kupeana zawadi huku pindi chakula kinapokuwa na harufu nzuri, na ikajulikana hali ya jirani.

Himizo la kutenda wema na kila kinachowezekana hata kikiwa kidogo, na kuingiza furaha kwa waislamu.

التصنيفات

Suluhisho na hukumu za ujirani.