Haingii peponi mfitinishaji

Haingii peponi mfitinishaji

Imepokewa kutoka kwa Hudhaifa -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- amesema: Nilimsikia Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- akisema: "Haingii peponi mfitinishaji".

[Sahihi] [Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim]

الشرح

Anaeleza Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- kuwa mmbea anayehamisha maneno kati ya watu kwa lengo la kuwavuruga kati yao yakuwa anastahiki adhabu kwa kutoingia peponi.

فوائد الحديث

Umbea ni katika madhambi makubwa.

Katazo la umbea; kwani ndani yake kuna kuwavuruga watu na madhara baina ya mtu na mtu na jamii mzima.

التصنيفات

Tabia mbovu.