Amelaaniwa mwenye kumuingilia mke wake kinyume na maumbile

Amelaaniwa mwenye kumuingilia mke wake kinyume na maumbile

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Huraira -radhi za Allah ziwe juu yake- amesema: Amesema: Mtume -rehema na amani ziwe juu yake-: "Amelaaniwa mwenye kumuingilia mke wake kinyume na maumbile".

[Ni nzuri]

الشرح

Anamtahadharisha Mtume rehema na amani ziwe juu yake mwanaume kumuingilia mkewe katika utupu wake wa nyuma; kuwa amelaaniwa na amefukuzwa kutoka katika rehema ya Mwenyezi Mungu, nalo ni dhambi katika madhambi makubwa.

فوائد الحديث

Uharamu wa kuwaingilia nyuma wanawake.

Kustarehe na mke sehemu yoyote katika mwili wake isiyokuwa nyuma inafaa.

Muislamu anamuingilia mwanamke katika tupu yake ya mbele kama alivyomuamrisha Mwenyezi Mungu; na ama kwa nyuma kuna kuharibu maumbile, na kupoteza kizazi, na kwenda kinyume na asili salama ya viumbe hai, na kuna madhara makubwa kati ya wanandoa.

التصنيفات

Adabu za Ndoa.