إعدادات العرض
Ya kwamba Mtume rehema na amani ziwe juu yake pindi alipomuelekeza kwenda Yemen alimuamrisha achukue miongoni mwa ng'ombe katika kila thelathini ndama alianza kufuatana na ng'ombe wengine, wa kiume au kike
Ya kwamba Mtume rehema na amani ziwe juu yake pindi alipomuelekeza kwenda Yemen alimuamrisha achukue miongoni mwa ng'ombe katika kila thelathini ndama alianza kufuatana na ng'ombe wengine, wa kiume au kike
Kutoka kwa Muadhi radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake: Ya kwamba Mtume rehema na amani ziwe juu yake pindi alipomuelekeza kwenda Yemen alimuamrisha achukue miongoni mwa ng'ombe katika kila thelathini ndama alianza kufuatana na ng'ombe wengine, wa kiume au kike, na katika kila arobaini mwenye miaka miwili, na kutoka kwa kila anayeishi humo asiye muislamu Dinari au kitu chenye thamani sawa na Dinari kama Maafiri, nazo ni nguo hutengenezwa Yemen.
الترجمة
العربية Bosanski English فارسی Français Русский हिन्दी 中文 Bahasa Indonesia اردو Kurdî Português دری Македонски Tiếng Việt Magyar ქართული বাংলা ไทย অসমীয়া Hausa Nederlands ਪੰਜਾਬੀالشرح
Mtume rehema na amani ziwe juu yake alimtuma Muadhi bin Jabali radhi za Allah ziwe juu yake kwenda Yemen kwa ajili ya kuwafundisha watu na kuwafikishia ujumbe, na miongoni mwa yale aliyomuamrisha achukue kutoka kwa Waislamu zaka za ng'ombe zao katika kila ng'ombe thelathini achukue dume moja au ng'ombe aliyeanza kufuatana na wengine machungani; naye ni yule aliyetimiza mwaka moja, na katika kila ng'ombe arobaini achukue ng'ombe mkamilifu; naye ni yule aliyetimiza miaka miwili. Na achukue jizia (kodi) kutoka kwa watu wa kitabu, Mayahudi na Wakristo, kwa kila mwanaume aliyebalehe, Dinari, au kinacholingana na Dinari katika nguo za Yemen ziitwazo: Maafari.فوائد الحديث
Jizia haichukuliwi isipokuwa kwa yule aliyebalehe; kwa sababu kigezo cha mtu asiyechukuliwa kodi ni: Ni yule ambaye haitakiwi kumuua akitekwa: Kama mtoto mdogo, na mwanamke, na wengineo.
Jizia makadirio yake yanarudi katika jitihada za kiongozi, kwa sababu zinatofautiana kulingana na kutofautiana kwa maeneo na zama, na utajiri na ufakiri, na ushahidi juu ya hilo nikuwa Mtume rehema na amani ziwe juu yake ndiye aliyetoa makadirio hayo kwa watu wa Yemen, akasema kumwambia Muadhi: "Chukua kwa kila aliyebalehe Dinari", wakati huo huo jizia iliongezeka katika makadirio ya Omari radhi za Allah ziwe juu yake wakati alipoweka kiwango kwa watu wa Sham.l
Kutilia umuhimu ukusanyaji wa zaka, na kumuwakilisha mwenye kukusanya ni katika majukumu ya kiongozi.
Tabii: Ni yule aliyetimiza mwaka mmoja, na akaingia mwaka wa pili, na ameitwa tabii; kwa sababu bado anamfuata mama yake.
Dinari: Ni pesa ya dhahabu, na Dinari ya kislamu: Uzito wake ni gramu nne na robo ya dhahabu (4.25gm).
التصنيفات
Zakkah ya wanyama wafugwao.