Hakuna watu wowote watasimama katika kikao ambacho hawamtaji Mwenyezi Mungu Mtukufu ndani yake, isipokuwa watanyanyuka mithili ya mzoga wa punda, na wanakua na majuto

Hakuna watu wowote watasimama katika kikao ambacho hawamtaji Mwenyezi Mungu Mtukufu ndani yake, isipokuwa watanyanyuka mithili ya mzoga wa punda, na wanakua na majuto

Kutoka kwa Abuu Huraira -radhi za Allah ziwe juu yake- amesema: Amesema Mtume -rehema na amani ziwe juu yake-: "Hakuna watu wowote watasimama katika kikao ambacho hawamtaji Mwenyezi Mungu Mtukufu ndani yake, isipokuwa watanyanyuka mithili ya mzoga wa punda, na wanakua na majuto".

[Sahihi] [Imepokelewa na Abuu Daud]

الشرح

Ameeleza Mtume rehema na amani ziwe juu yake yakwamba hakuna kundi la watu watakaokaa katika kikao kisha wakanyanyuka katika kikao hicho haliyakuwa hawajamtaja Mwenyezi Mungu ndani yake isipokuwa watanyanyuka katika mfano wa mzoga wa punda katika kunuka na uchafu; na hii ni kwa sababu walishughulika na mazungumzo wakaacha kumtaja Mwenyezi Mungu, na kikao hicho kwao kitakuwa ni masikitiko siku ya Kiyama na ni mapungufu na majuto kwao.

فوائد الحديث

Yaliyotajwa katika kutahadharisha kughafilika na kumtaja Mwenyezi Mungu hayaishii katika kikao pekee, bali yanaenea mahala pengine, amesema Imam Nawawi: Ni machukizo kwa atakayekaa mahali aondoke kabla hajamtaja Mwenyezi Mungu Mtukufu ndani yake.

Masikitiko yatakayotokea kwao siku ya Kiyama: Ima kwa kupitwa na malipo na thawabu kwa kutofaidika na wakati katika kumtii Mwenyezi Mungu, na ima kwa madhambi na adhabu kwa kuutumia wakati kwa kumuasi Mwenyezi Mungu.

Tahadhari hii ni pale kujisahau kutakapokuwa ni kwa mambo ya halali, vipi kwa vikao vya haramu ambavyo ndani yake kuna utesi na usengenyaji na mengineyo?!.

التصنيفات

Fadhila za Adh-kaar.