Tulikatazwa kusindikiza jeneza, na hatukusisitiziwa katazo hilo

Tulikatazwa kusindikiza jeneza, na hatukusisitiziwa katazo hilo

Kutoka kwa Ummu Atwiya radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake amesema: Tulikatazwa kusindikiza jeneza, na hatukusisitiziwa katazo hilo.

[Sahihi] [Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim]

الشرح

Anaeleza Ummu Atwiya Muanswari (mzaliwa wa Madina) radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake, ya kwamba Mtume rehema na amani ziwe juu yake aliwakataza wanawake kusindikiza jeneza; na hii ni kwa sababu ya mitihani inayohofiwa juu yao, na uchache wa subira yao, kisha akaeleza radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake kuwa Mtume rehema na amani ziwe juu yake hakutilia mkazo katika katazo hili kama anavyofanya katika matakazo mengine.

فوائد الحديث

Kuwakataza wanawake kusindikiza jeneza, nalo ni katazo la jumla la kulisindikiza, kuanzia linapoandaliwa na kuswaliwa, na mpaka makaburini linapozikwa.

Sababu ya katazo, ni kwa sababu wanawake hawawezi kuhimili mfano wa sehemu kama hizi zenye kuhuzunisha, na mazingira yenye kuathiri; huenda kukaonekana kwao kulalamika, na kupaparika, mambo yanayokwenda kinyume na subira inayohitajika.

Asili ya katazo huwa ni uharamu, isipokuwa Ummu Atwiya radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake alielewa kutokana na viashiria vya hali halisi kuwa katazo lao la kusindikiza jeneza si la mkazo uliosisitizwa, lakini zimekuja hadithi zilizoonyesha kutilia mkazo katika kusindikiza jeneza zaidi kuliko jinsi inavyoonyesha hadithi hii.

التصنيفات

Dalili za kimatamshi na namna ya kudadavua., Kutembelea Makaburi.