Mswaki ni usafi wa kinywa, humridhisha Mola

Mswaki ni usafi wa kinywa, humridhisha Mola

Kutoka kwa Aisha -Radhi za Allah ziwe juu yake- amesema: Amesema Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake-: "Mswaki ni usafi wa kinywa, humridhisha Mola".

[Sahihi] [Imepokelewa na An-Nasaaiy]

الشرح

Anatueleza Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- kuwa kusafisha meno kwa kijiti cha mti wa Arak na mfano wake husafisha kinywa kutokana na uchafu na harufu mbaya, Nakuwa ni katika sababu za kumridhisha Allah Mtukufu kwa mja; kwa sababu ndani yake kuna kumtii Allah na kuitika amri yake, na pia kuna usafi anaoupenda Allah Mtukufu.

فوائد الحديث

Ubora wa mswaki, na Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- kuuhimiza umma wake kukithirisha kupiga

Katika mswaki ni bora kutumia kijiti cha mti wa Arak, na kutumia miswaki ya brashi na dawa ya meno hukaa badala yake.

التصنيفات

Sunna za Kimaumbile., Sunna za Kimaumbile.