Nilisema: Ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu ni kupi kunusurika? Akasema: "Shika ulimi wako, na ikutoshe nyumba yako, na lia kwa ajili ya makosa yako

Nilisema: Ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu ni kupi kunusurika? Akasema: "Shika ulimi wako, na ikutoshe nyumba yako, na lia kwa ajili ya makosa yako

Kutoka kwa Ukba bin Aamir Al-Juhaniy -radhi za Allah ziwe juu yake amesema: Nilisema: Ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu ni kupi kunusurika? Akasema: "Shika ulimi wako, na ikutoshe nyumba yako, na lia kwa ajili ya makosa yako".

[Sahihi]

الشرح

Ukba bin Aamiri alimuuliza Mtume rehema na amani ziwe juu yake kuhusu sababu za muumini kuokoka katika dunia na Akhera? Akasema rehema na amani ziwe juu yake: Shikamana na mambo matatu: La kwanza: Hifadhi ulimi wako katika yale yasiyokuwa na kheri ndani yake, na kuzungumza kila shari, na usitamke ila la kheri. La pili: Baki nyumbani kwako ili umuabudu Mwenyezi Mungu katika nyakati za faragha, na ujishughulishe na kumtii Mwenyezi Mungu Mtukufu kwa ibada, na jitenge nyumbani kwako na fitina. La tatu: Lia na ujute na utubie kwa yale uliyoyatenda katika madhambi.

فوائد الحديث

Pupa ya Maswahaba katika kujua njia za kusalimika.

Kumebainishwa sababu za kusalimika katika Dunia na Akhera.

Himizo la mtu kushughulika na nafsi yake anaposhindwa kumnufaisha mtu mwingine, au akahofia madhara juu ya dini yake na nafsi yake endapo atachanganyikana na watu.

Hapa kuna ishara ya kuipa kipaumbele nyumba, na hasa hasa wakati wa fitina, kwani ni katika nyenzo za kuihifadhi dini.

التصنيفات

Adabu ya mazungumzo na kunyamaza., Toba