Atakayefunga Ramadhani kwa imani na kutaraji malipo toka kwa Allah, atasamehewa madhambi yake yaliyotangulia

Atakayefunga Ramadhani kwa imani na kutaraji malipo toka kwa Allah, atasamehewa madhambi yake yaliyotangulia

Imepokewa Kutoka kwa Abuu Huraira -Radhi za Allah ziwe juu yake- amesema: Amesema Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake-: "Atakayefunga Ramadhani kwa imani na kutaraji malipo toka kwa Allah, atasamehewa madhambi yake yaliyotangulia"

[Sahihi] [Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim]

الشرح

Anaeleza Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- kuwa atakayefunga mwezi wa Ramadhani kwa kumuamini Mwenyezi Mungu, na kwa kuitakidi ulazima wa swaumu na yale aliyoyaahidi Mwenyezi Mungu Mtukufu kwa wafungaji kuwa na malipo makubwa na thawabu, akikusudia kupata radhi za Allah Mtukufu si kwa kutaka kujionyesha au kusikika, yatasamehewa kwake madhambi yake yaliyopita.

فوائد الحديث

Fadhila za kutakasa matendo, na umuhimu wake katika funga ya Ramadhani na amali njema nyinginezo.

التصنيفات

Ubora na Fadhila za Funga.