Pindi atakapaowakusanya Mwenyezi Mungu wa mwanzo na wa mwisho siku ya Kiyama itanyanyuliwa bendera kwa kila haini, patasemwa: Hii ndio hiana ya fulani bin fulani

Pindi atakapaowakusanya Mwenyezi Mungu wa mwanzo na wa mwisho siku ya Kiyama itanyanyuliwa bendera kwa kila haini, patasemwa: Hii ndio hiana ya fulani bin fulani

Kutoka kwa bin Omari radhi za Allah ziwe juu yao yeye na baba yake, amesema: Amesema Mtume wa Mwenyezi Mungu rehema na amani ziwe juu yake: "Pindi atakapaowakusanya Mwenyezi Mungu wa mwanzo na wa mwisho siku ya Kiyama itanyanyuliwa bendera kwa kila haini, patasemwa: Hii ndio hiana ya fulani bin fulani".

[Sahihi] [Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim]

الترجمة

ar bn bs en es fa fr id ru tl tr ur zh hi vi ug ha pt ml ku nl as gu si hu ka ro

الشرح

Anaeleza Mtume rehema na amani ziwe juu yake ya kwamba Mwenyezi Mungu Mtukufu siku ya Kiyama atakapowakusanya wa mwanzo na wa mwisho kwa ajili ya hesabu, atasimika kwa kila haini ambaye hakutimiza ahadi aliyokubaliana nayo kwa Mwenyezi Mungu au pamoja na watu, alama ambayo atamfedhehesha kwayo mbele za watu kwa sababu ya hiana yake, na kutanadiwa juu yake siku hiyo: Hii ndio hiana ya fulani bin fulani; kwa ajili ya kutangaza ubaya wa kitendo chake mbele ya waliokusanyika katika uwanja halaiki (mahashari).

فوائد الحديث

Uharamu wa hiana na kwamba hilo ni katika madhambi makubwa; kwa sababu ndani yake kuna ahadi hii kali ya adhabu.

Hiana iliyosemwa katika hadithi inakusanya kila aliyekuamini juu ya damu, au heshima, au siri, au mali, kisha ukamfanyia hiana, na ukaenda kinyume na dhana yake katika kukuamini kwake.

Amesema Qurtubi: Hili ni tamko kutoka kwake linawahusu waarabu kwa sababu ya yale waliyokuwa wakiyafanya; kwani wao walikuwa wakinyanyua bendera nyeupe kwa ajili ya kutimiza ahadi, na kwa usaliti bendera nyeusi, ili wamlaumu haini na wamkemee, hadithi ikapelekea kutokea mfano wa hilo kwa haini; ili awe mashuhuri kwa sifa yake hiyo siku ya Kiyama, na watamsema kwa ubaya waliosimama katika uwanja huo.

Amesema bin Hajari: Na katika hadithi hii nikuwa watu siku ya Kiyama wataitwa kwa ubini wa baba zao; kwa kauli yake aliposema: "Huu ni usaliti wa fulani bin fulani".

التصنيفات

Tabia mbovu., Adabu za Jihadi.