Yakwamba Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- Amekataza kuweka nadhiri, na akasema: Hakika nadhiri haiji kwa kheri, na hakika hutolewa kwayo (vilivyo) kwa bahili

Yakwamba Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- Amekataza kuweka nadhiri, na akasema: Hakika nadhiri haiji kwa kheri, na hakika hutolewa kwayo (vilivyo) kwa bahili

Kutoka kwa bin Omar Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yao- Kutoka kwa Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- "Yakwamba yeye Amekataza kuweka nadhiri, na akasema: Hakika nadhiri haiji kwa kheri, na hakika hutolewa kwayo (vilivyo) kwa bahili".

[Sahihi] [Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim]

الشرح

Amekataza Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- kuweka nadhiri, na akatoa sababu ya katazo lake kuwa haiji kwa kheri; na hiyo ni kwasababu ya yale yanayoambatana nayo, ikiwemo mtu kujiwajibishia juu ya nafsi yake kitu ambacho yeye ana uhuru nacho, ikahofiwa huenda akafanya uzembe katika kukitekeleza, akajiingiza katika madhambi, na kile kilichomo cha kutaka kumpa badala Mwenyezi Mungu -Mtukufu- katika kushikamana na ibada kwa kuweka sharti la kupata unachotafuta, au kuondolewa maudhi. Na huenda akadhani -Mwenyezi Mungu atuepushe- kuwa amejibu ombi lake ili yeye atekeleze ibada yake. kwasababu hizi na nyinginezo, ndio maana amekataza Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake-; kwa kuthamini usalama, na kwa kutamani ukarimu wa Mwenyezi Mungu -Mtukufu- bila mbadala wala kumuwekea sharti, bali kwa matarajio na dua. Na hakuna faida yoyote katika nadhiri, isipokuwa ni kutolewa kupitia nadhiri vilivyo kwa mtu bahili, ambaye hatekelezi isipokuwa yale yaliyomuwajibikia kwake kuyafanya na ikawa ni faradhi kwake kuyatekeleza, akayafanya kwa kulazimishwa, tena kwa uzito, na akiwa hana misingi ya kufanya matendo, ambayo ni nia njema, na shauku juu ya yale yaliyoko kwa Mwenyezi Mungu -Mtukufu-.

التصنيفات

Viapo na Nadhiri.