Fanyeni haraka kufanya matendo kuna fitina nzito kama kipande cha usiku wa giza,

Fanyeni haraka kufanya matendo kuna fitina nzito kama kipande cha usiku wa giza,

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Huraira -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- yakwamba Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- amesema: "Fanyeni haraka kufanya matendo kuna fitina nzito kama kipande cha usiku wa giza, anaamka mtu akiwa muislamu anafika jioni akiwa kafiri, na anashinda akiwa muumini anaamka asubuhi akiwa kafiri, anauza dini yake kwa thamani ndogo ya dunia"

[Sahihi] [Imepokelewa na Imamu Muslim]

الشرح

Mtume rehema na amani ziwe juu yake anamtaka Muumini kufanya hima na kufanya mambo mengi ya kheri kabla hayajashindikana, na akashughulishwa na kuja kwa fitna na mambo yenye kutatiza yanayoweza kuzuia kufanya matendo mema, na kuyaziba, na hali ni kwamba, ni giza kama kipande cha usiku ambao ndani yake haki imechanganyika na batili, na kukawawia vigumu watu kutofautisha baina yake, na kwa sababu ya ukali wake (Fitina hiyo), mtu huchanganyikiwa kiasi cha kuamka muumini, na kufika jioni ni kafiri, kushinda Muumini na kufika asubuhi kawa kafiri, anaiacha dini yake kwa starehe za muda mfupi za dunia.

فوائد الحديث

Ni lazima kushikamana na dini, na kwenda mbio katika matendo mema kabla ya vikwazo kuzuia hilo.

Hii ni ishara ya mfuatano wa majaribu yenye kupoteza katika zama za mwisho, na kwamba wakati wowote fitina moja inapotoweka, fitina ingine linafuata.

Ikiwa dini ya mtu ni dhaifu na akaiacha kwa kubadilishana na mambo ya kidunia, kama vile pesa au vitu vingine, hii ni sababu ya kupotoka kwake, kuacha dini, na kuingia kwake kwenye vishawishi na fitina.

Kuna ushahidi katika Hadithi kwamba matendo mema ni njia ya kuokoka na fitina.

Kuna aina mbili za fitina: Fitina ya shubuha (Mambo yenye utata), na tiba yake ni elimu, na fitina ya matamanio, na tiba yake ni imani na subira.

Hadithi inaashiria kuwa mwenye matendo kidogo, fitina kwake ni nyepesi zaidi, na mwenye matendo mengi anatakiwa asihadaike na alichonacho, bali aongeze zaidi.

التصنيفات

Sehemu ya Imani.