إعدادات العرض
Hakuna waislamu wawili watakaokutana wakapeana mikono isipokuwa watasamehewa kabla hawajaachana
Hakuna waislamu wawili watakaokutana wakapeana mikono isipokuwa watasamehewa kabla hawajaachana
Kutoka kwa Barraa -radhi za Allah ziwe juu yake- amesema: Amesema Mtume wa Mwenyezi Mungu -rehema na amani ziwe juu yake: "Hakuna waislamu wawili watakaokutana wakapeana mikono isipokuwa watasamehewa kabla hawajaachana".
الترجمة
العربية বাংলা Bosanski English Español فارسی Français Bahasa Indonesia Русский Tagalog Türkçe اردو 中文 हिन्दी සිංහල ئۇيغۇرچە Hausa Kurdî Português অসমীয়া Tiếng Việt ગુજરાતી Nederlands አማርኛ മലയാളം Română ไทยالشرح
Ameeleza Mtume rehema na amani ziwe juu yake: Kuwa hakuna waislamu wawili watakaokutana njiani na mfano wake wakasalimiana kwa kupeana mikono isipokuwa watasamehewa kabla hawajaachana kwa viwiliwili au kwa kumaliza kupeana mikono.فوائد الحديث
Sunna ya kupeana mikono wakati wa kukutana, na himizo juu yake.
Amesema Manawi: Na sunna haipatikani isipokuwa kwa kuweka mkono wa kulia katika mkono wa kulia kiasi kwamba hakuna udhuru.
Himizo la kusambaza salamu, na kumebainishwa ukubwa wa malipo ya kumpa mkono muislamu ndugu yake muislamu.
Kunavuliwa katika hadithi kupeana mikono kwa haramu, kama kumpa mkono mwanamke wa kando.