Yakwamba Mtume -rehema na amani ziwe juu yake- alikuwa anapo swali anatanua kati ya mikono yake mpaka unaonekana weupe wa kwapa zake

Yakwamba Mtume -rehema na amani ziwe juu yake- alikuwa anapo swali anatanua kati ya mikono yake mpaka unaonekana weupe wa kwapa zake

Kutoka kwa Abdallah bin Maliki bin Buhaina radhi za Allah ziwe juu yake: Yakwamba Mtume -rehema na amani ziwe juu yake- alikuwa anapo swali anatanua kati ya mikono yake mpaka unaonekana weupe wa kwapa zake.

[Sahihi] [Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim]

الشرح

Alikuwa rehema na amani zimshukie anaposwali, anaikunjua mikono yake wakati wa kusujudu. Alisogeza kila mkono kutoka upande wa karibu yake, kama mbawa mbili, mpaka rangi ya ngozi ya makwapa yake inaonekana; Hii ni katika kupitiliza kuitanua mikono na kuitenganisha na mbavu zake.

فوائد الحديث

Mkao huu unapendeza katika sijida, nao ni kuweka mbali vikwapa na mbavu.

Maamuma ambaye jirani yake anakereka kwa kutanua kwake mikono; si sheria kwake kufanya hivyo.

Katika kutanua mikono katika sijida, kuna hekima na faida nyingi, miongoni mwake ni: kuonyesha uchangamfu na hamu ya kusali, na kwamba ikiwa mtu ataegemea viungo vyote katika sijida, kila kiungo kitapata sehemu yake ya ibada. Ikasemwa kuwa: Hekima katika hili ni kuwa ni sawa na unyenyekevu, na inafaa zaidi katika kuweka paji la uso na pua karibu na ardhi, na pia ili kila kiungo kiweze kutofautishwa peke yake.

التصنيفات

Muongozo wake Mtume Mtume Rehma na za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake amani katika swala