إعدادات العرض
1- Nilisali pamoja na Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- rakaa mbili kabla ya adhuhuri, na rakaa mbili baada yake, na rakaa mbili baada ya Ijumaa, na rakaa mbili baada ya magharibi, na rakaa mbili baada ya ishaa
2- Yakwamba Nabii -Rehema na Amani ziwe juu yake- alikuwa safarini, akaswali swala ya ishaa ya mwisho, akasoma katika moja ya rakaa mbili kwa sura ya wattin wazzaitun, sijawahi kumsikia yeyote mwenye sauti nzuri au kisomo kizuri zaidi yake
3- Yakwamba Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- alikuwa anapo swali anatanua kati ya mikono yake mpaka unaonekana weupe wa kwapa lake
4- Alikuwa Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- akiitembelea msikiti wa Qubaa kwa kipando na pia kwa miguu, anaswali ndani yake rakaa mbili