, atamuingiza Mwenyezi Mungu peponi kulingana na yale aliyokuwa nayo katika matendo

, atamuingiza Mwenyezi Mungu peponi kulingana na yale aliyokuwa nayo katika matendo

Kutoka kwa Ubada bin -Radhi za Allah ziwe juu yake- kutoka kwa Mtume Rehema na amani za Allah ziwe juu yake amesema: "Atakaye shuhudia kuwa hapana Mola isipokuwa Mwenyezi Mungu yeye pekee asiye na mshirika nakuwa Muhammadi ni mjumbe wake na ni mja wake, nakuwa Issa ni mja wa Mwenyezi Mungu na Mtume wake na neno lake alilolipeleka kwa Mariam na ni roho toka kwake, na pepo ni kweli na moto ni kweli, atamuingiza Mwenyezi Mungu peponi kulingana na yale aliyokuwa nayo katika matendo".

[Sahihi] [Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim]

الشرح

Anatueleza Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- yakuwa atakayetamka neno la tauhidi kwa kujua maana yake, kwa kuyafanyia kazi madhumuni yake, na akashuhudia utumwa wa Muhammadi -Rehema na amani ziwe juu yake- na ujumbe wake, na akakiri utumwa wa Issa na ujumbe wake, Na kuwa Mwenyezi Mungu alimuumba kwa kauli yake "Kuwa" na akawa, na kuwa yeye ni roho miongoni mwa roho alizoziumba Mwenyezi Mungu, Na akamtenga mbali mama yake kwa yale waliyomnasibisha nayo Mayahudi, Nakuwa atakayeamini pepo kuwa ni kweli, na kuwa Moto ni kweli, akaitakidi uwepo wake, nakuwa hizo ni neema za Mwenyezi Mungu na adhabu yake, Na atakayekufa katika imani hiyo; basi mafikio yake ni Peponi hata kama alikuwa mzembe katika ibada, na anamadhambi.

فوائد الحديث

Mwenyezi Mungu Mtukufu kamuumba Issa mwana wa Mariamu kwa neno (Kuwa) bila baba.

Kinachowakusanya pamoja kati ya Issa (Yesu) na Muhammadi amani iwe juu yao wote ni kuwa ni waja wa Mwenyezi Mungu na Mitume wake, basi wao wote wawili ni Mitume hawasemi uongo, na ni waja wala hawaabudiwi.

Ubora wa tauhidi na kufuta kwake madhambi, nakuwa mafikio ya mtu wa tauhidi ni Peponi, hata kama yakajitokeza kwake baadhi ya madhambi.

التصنيفات

Kumuamini Allah mwenye nguvu alie tukuka, Kuamini siku ya mwisho, Sifa za pepo na moto.