“Je, nisiwaambieni matendo bora zaidi kwenu, na masafi zaidi mbele ya Mfalme wenu, na yatakayo kunyanyueni juu zaidi katika daraja zenu

“Je, nisiwaambieni matendo bora zaidi kwenu, na masafi zaidi mbele ya Mfalme wenu, na yatakayo kunyanyueni juu zaidi katika daraja zenu

Kutoka kwa Abuu Dardaa -Radhi za Allah ziwe juu yake- Amesema: Amesema Mtume wa Mwenyezi Mungu -Rehema na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake: “Je, nisiwaambieni matendo bora zaidi kwenu, na masafi zaidi mbele ya Mfalme wenu, na yatakayo kunyanyueni juu zaidi katika daraja zenu, na bora kwenu kuliko kutoa dhahabu na pesa, na bora kwenu kuliko hata kukutana na adui yenu na mkapiga shingo zao na wakapiga shingo zenu?" Wakasema: Ndiyo. Akasema: “Ni kumtaja Mwenyezi Mungu".

[Sahihi]

الشرح

Maswahaba walimuuliza Mtume rehema na amani ziwe juu yake: . Hivi je mnata nikuelezeni na nikufundisheni amali bora zaidi kuliko zote katika amali zenu, na yenye utukufu kuliko zote na yenye kukua zaidi na safi zaidi na takatifu zaidi mbele ya Mwenyezi Mungu Mfalme Aliyetukuka? . na yenye nafasi ya juu zaidi katika nafasi zenu za peponi? na ambayo ni bora zaidi kwenu kuliko kutoa sadaka ya Dhahabu na fedha? na bora kwenu kuliko hata kukutana na makafiri vitani, mkapiga shingo zao, na wakapiga shingo zenu? Maswahaba wakasema: Ndio tunalitaka hilo. Akasema rehema na amani ziwe juu yake: Ni kumtaja Mwenyezi Mungu katika nyakati zote na katika mikao yote na hali zote.

فوائد الحديث

Nikuwa kudumu katika kumtaja Mwenyezi Mungu Mtukufu kwa wazi na kwa siri ni katika mambo makubwa yanayomuweka mtu karibu na Mola wake, na yenye manufaa makubwa mbele ya Mwenyezi Mungu Mtukufu.

Vitendo vyote viliwekwa ili kumkumbuka Mwenyezi Mungu Mtukufu, amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu: "Na simamisha sala kwa kunikumbuka". Naye, rehema na amani za Mwenyezi Mungu zimshukie, amesema: "Kuizunguka Al-Kaaba na baina ya Safa na Marwah na kurusha mawe kulikusudiwa tu kumtaja Mwenyezi Mungu" Imepokelewa na Abu Daudi na Tirmidhiy.

Al-Izzi bin Abdul Salam amesema katika Qawaid yake: Hadithi hii inaashiria kwamba malipo hayatokani na kiwango cha uchovu katika ibada zote, bali Mwenyezi Mungu Mtukufu anaweza kulipa zaidi kwa matendo madogo kuliko mengi, hivyo malipo yanatokana na tofauti za daraja katika utukufu.

Al-Munawiy amesema katika Faidh al-Qadir: Hadithi hii inafasiriwa kuwa dhikri imekuwa bora kwa wale walioambiwa kuifanya, kwakuwa, na lau kama mtu shupavu na shujaa angeliambiwa kuifanya na yakapatikana manufaa katika Uislamu basi ingeitwa Jihadi, au tajiri ambaye mali yake inawanufaisha masikini, basi ingeitwa sadaka, au mtu mwenye uwezo wa kuhiji, basi ingeitwa Hija, au mtu mwenye wazazi wawili, basi ingeitwa wema kwa wazazi, na kupitia kwake inapatikana taufiki kati ya habari na habari.

Dhikiri iliyokamilika zaidi ni ile ambayo ulimi umetamka ikiwa pamoja na mazingatio ya moyo, kisha ile iliyomo moyoni peke yake kama tafakuri, kisha inayokuwa kwa ulimi peke yake, na kila moja ina ujira, In shaa Allah.

Muislamu kudumu na dhikiri zenye kuendana na hali mbali mbali kama asubuhi na jioni, na kuingia msikitini na nyumbani na chooni na wakati wa kutoka, na nyinginezo, hii inamfanya kuwa miongoni mwa wenye kumtaja Mwenyezi Mungu kwa wingi.

التصنيفات

Fadhila za Adh-kaar.