Muislamu atakapoulizwa kaburini anashuhudia kuwa hapana Mola apasaye kuabudiwa kwa haki isipokuwa Mwenyezi Mungu, nakuwa Muhammadi ni Mjumbe wa Mwenyezi Mungu

Muislamu atakapoulizwa kaburini anashuhudia kuwa hapana Mola apasaye kuabudiwa kwa haki isipokuwa Mwenyezi Mungu, nakuwa Muhammadi ni Mjumbe wa Mwenyezi Mungu

kutoka kwa Albaraa bin Aazib Radhi za Allah ziwe juu yake- hakika Mtume Rehema na amani za Allah ziwe juu yake alisema: "Muislamu atakapoulizwa kaburini anashuhudia kuwa hapana Mola apasaye kuabudiwa kwa haki isipokuwa Mwenyezi Mungu, nakuwa Muhammadi ni Mjumbe wa Mwenyezi Mungu", Hiyo ndiyo kauli yake Mtukufu: "Huwapa umakinifu Mwenyezi Mungu wale walioamani kwa kauli thabiti katika maisha ya dunia na katika akhera" [Ibrahim: 27].

[Sahihi] [Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim]

الشرح

Muumini ataulizwa kaburini, watamuuliza Malaika wawili waliopangiwa kufanya hivyo, nao ni Munkari na Nakiri, kama walivyotajwa katika Hadithi kadhaa, atashuhudia kuwa hapana mola apasaye kuabudiwa kwa haki isipokuwa Mwenyezi Mungu na kuwa Muhammadi ni Mjumbe wa Mwenyezi Mungu, Akasema Mtume rehema na amani ziwe juu yake, hii ndio kauli thabiti aliyoisema Mwenyezi Mungu: "Huwapa umakinifu Mwenyezi Mungu wale walioamani kwa kauli thabiti katika maisha ya dunia na katika akhera" [Surat Ibrahim: 27].

فوائد الحديث

Nikuwa maswali ya kaburini ni kweli yapo.

Fadhila ya Mwenyezi Mungu Mtukufu juu ya waja wake waumini katika dunia na akahera anawapa nguvu kwa kauli thabiti.

Ubora wa shahada ya tauhidi na kufa juu yake.

Mwenyezi Mungu kumpa thabati (nguvu) Muumini katika dunia ni kwa kumpa msimamo katika imani, na kutembea katika njia iliyonyooka, na wakati wa kufa kwa kufa katika tauhidi, na kaburini wakati akiulizwa na Malaika wawili.

التصنيفات

Maisha ya Barzakhi(Baada ya kufa)