Hakika Mwenyezi Mungu ameniondolea mimi kwa umma wangu (madhambi ya) kukosea na kusahau, na yale waliyolazimishwa

Hakika Mwenyezi Mungu ameniondolea mimi kwa umma wangu (madhambi ya) kukosea na kusahau, na yale waliyolazimishwa

Kutoka kwa Abdillah bin Abbas -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- Hadithi Marfu'u: "Hakika Mwenyezi Mungu ameniondolea mimi kwa umma wangu (madhambi ya) kukosea na kusahau, na yale waliyolazimishwa".

[Ni sahihi kwa njia zake na ushahidi wake] [Imepokelewa na Ibnu Maajah]

الشرح

Miongoni mwa huruma ya Mwenyezi Mungu Mtukufu kwa umma huu ni kuusamehe madhambi ya kukosea -Nayo ni yale ambayo hawajakusudia miongoni mwa maasi- na kusahau wajibu wao au kufanya maharamisho, lakini baadaye akikumbuka wajibu wake anaufanya, hivyo hivyo hata yale waliyolazimishwa na wakatezwa nguvu kuyafanya katika maasi na makosa ya jinai, Akasema Mwenyezi Mungu Mtukufu: "Na hakukufanyieni juu yenu uzito katika dini".

التصنيفات

Kumuamini Allah mwenye nguvu alie tukuka