Ya kwamba mtu mmoja alimuuliza Mtume rehema na amani zimfikie: Ni Uislamu upi bora? Akasema: "Ni, ulishe chakula, na utoe salamu kwa unayemjua na usiyemjua

Ya kwamba mtu mmoja alimuuliza Mtume rehema na amani zimfikie: Ni Uislamu upi bora? Akasema: "Ni, ulishe chakula, na utoe salamu kwa unayemjua na usiyemjua

Kutoka kwa Abdallah Bin Amri -Radhi za Allah ziwe juu yake na baba yake-: Ya kwamba mtu mmoja alimuuliza Mtume rehema na amani zimfikie: Ni Uislamu upi bora? Akasema: "Ni, ulishe chakula, na utoe salamu kwa unayemjua na usiyemjua".

[Sahihi] [Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim]

الشرح

Aliulizwa Mtume rehema na amani zimfikie: Ni jambo lipi katika Uislamu ni bora? Akataja mambo mawili: La kwanza: Kukirithirisha kuwalisha masikini, na inaingia hapa sadaka na zawadi na kuwakirimu wageni na walima (harusi), na inatiliwa mkazo fadhila ya kulisha masikini katika nyakati za njaa na wakati wa bidhaa kupanda bei. La pili: Kumpa salamu kila muislamu, unayemjua na usiyemjua.

فوائد الحديث

Pupa ya Masahaba katika kuyajua mambo yenye manufaa katika Dunia na Akhera.

Salamu na kulisha chakula ni miongoni mwa amali bora katika Uislamu; kwa sababu ya fadhila zake na uhitaji wa watu juu ya chakula katika wakati wote.

Kwa mambo haya mawili ihisani (wema) unakuwa kwa kauli na vitendo, nao ndio wema uliokamilika zaidi.

Mambo haya ni katika mambo yanayohusu maisha ya waislamu baina yao, na kuna mambo yanahusu mahusiano ya mja na Mola wake.

Kuanza kwa salamu ni maalumu kwa waislamu, haitolewi salamu kwa kumuanza asiyekuwa muislamu.

التصنيفات

Mambo mazuri na Adabu- Heshima., Adabu za kuto asalamu na kubisha Hodi.