إعدادات العرض
Kwa hakika miongoni mwa alama za Kiyama ni kuondolewa elimu, na kuzidi ujinga, na kukithiri uzinifu, unywaji pombe, na wanaume watakuwa wachache na wanawake watakuwa wengi mpaka itafikia wanawake hamsini kusimamiwa na mwanaume mmoja
Kwa hakika miongoni mwa alama za Kiyama ni kuondolewa elimu, na kuzidi ujinga, na kukithiri uzinifu, unywaji pombe, na wanaume watakuwa wachache na wanawake watakuwa wengi mpaka itafikia wanawake hamsini kusimamiwa na mwanaume mmoja
Imepokelewa kutoka kwa Anas -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake, amesema: Nitawahadithieni Hadithi nimeisikia kutoka kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu -Rehema na amani ziwe juu yake-, na hadithi hiyo hatowahadithia yeyote asiyekuwa mimi: Nimemsikia Mtume wa Mwenyezi Mungu -Rehema na amani ziwe juu yake anasema: "Kwa hakika miongoni mwa alama za Kiyama ni kuondolewa elimu, na kuzidi ujinga, na kukithiri uzinifu, unywaji pombe, na wanaume watakuwa wachache na wanawake watakuwa wengi mpaka itafikia wanawake hamsini kusimamiwa na mwanaume mmoja."
الترجمة
العربية English မြန်မာ Svenska Čeština ગુજરાતી አማርኛ Yorùbá Nederlands اردو Español Bahasa Indonesia ئۇيغۇرچە বাংলা Türkçe Bosanski සිංහල हिन्दी Tiếng Việt Hausa മലയാളം తెలుగు ไทย پښتو অসমীয়া Shqip دری Ελληνικά Български Fulfulde Italiano ಕನ್ನಡ Кыргызча Lietuvių Malagasy or Română Kinyarwanda Српски тоҷикӣ O‘zbek नेपाली Moore Kurdî Oromoo Wolof Soomaali Français Azərbaycan Tagalog Українська bm தமிழ் ქართული Deutsch Português Македонски Magyar فارسی Русский 中文الشرح
Anaweka wazi Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- kuwa katika alama za kukaribia Kiyama ni kuondolewa elimu ya sheria na kuondolewa kwake itakuwa ni kwa kufa wanachuoni. Na matokeo yake utazidi na utaenea ujinga, na uzinifu utaenea na uchafu, na unywaji pombe utazidi na idadi ya wanaume itapungua na ya wanawake itazidi; Mpaka itafikia hatua mwanaume mmoja atabeba mambo yao na kusimamia maslahi yao.فوائد الحديث
Kumewekwa wazi baadhi ya alama za Kiyama.
Kujua muda wa Kiyama ni katika mambo ya ghaibu (yasiyoonekana wala kujulikana) ni katika mambo ambayo Mwenyezi Mungu ameyaficha.
Himizo juu ya kujifunza elimu ya kisheria kabla ya kukosekana kwake.