Alikuwa Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- akitawadha kila wakati wa swala

Alikuwa Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- akitawadha kila wakati wa swala

Kutoka kwa Amri bin Aamiri kutoka kwa Anasi amesema: Alikuwa Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- akitawadha kila wakati wa swala, nikasema: Nyinyi mlikuwa mnafanya vipi? Akasema: Ulikuwa ukimtosha mmoja wetu udhu mmoja madam hajatengukwa.

[Sahihi] [Imepokelewa na Al-Bukhaariy]

الشرح

Alikuwa Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- akitawadha kwa kila swala ya faradhi hata kama hajatengukwa udhu; Na hii ni kwa sababu ya kupata malipo na fadhila. Na inafaa kwa mtu kuswali kwa zaidi ya swala moja kwa udhu mmoja madam bado yuko na udhu wake.

فوائد الحديث

Mwenendo uliodumu zaidi wa Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- ni kushika udhu kwa kila swala; ili kutaka ukamilifu zaidi.

Sunna ya kushika udhu kila wakati wa swala.

Inafaa kutekeleza zaidi ya swala moja kwa udhu mmoja.

التصنيفات

Fadhila - ubora wa kutawadha.