“Mfano wa rafiki mwema na rafiki muovu ni mfano wa mbeba miski na mfua vyuma

“Mfano wa rafiki mwema na rafiki muovu ni mfano wa mbeba miski na mfua vyuma

Na kutoka kwa Abuu Musa Radhi za Allah ziwe juu yake- kutoka kwa Mtume Rehema na amani za Allah ziwe juu yake amesema: “Mfano wa rafiki mwema na rafiki muovu ni mfano wa mbeba miski na mfua vyuma. Mbeba miski: atakukaribia utapata harufu nzuri ya marashi yake, au utanunua kwake, na ama mfua vyuma: Ima atachoma nguo zako, au utasikia harufu mbaya.”

[Sahihi] [Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim]

الشرح

Amepiga mfano Mtume rehema na amani ziwe juu yake, wa aina mbili za watu: Aina ya kwanza: Rafiki mwema anayemjulisha rafiki yake kwa Mwenyezi Mungu na yanayomridhisha, na kumsaidia katika utiifu, Mfano wake ni kama muuza miski, ima atakupa, au utanunua kwake, au utapata na kunusa harufu nzuri kutoka kwake. Aina ya pili: Rafiki na swahiba mbaya; Anayeziba njia ya Mwenyezi Mungu, na anasaidia katika kutenda maasi, na unaona wazi kwake matendo machafu, na wewe unasemwa vibaya kwa kufuatana naye na kukaa na mtu kama yeye. Mfano wake ni kama mhunzi apulizaye moto wake; ima itachoma nguo zako kutokana na cheche zake zinazoruka, au utasikia harufu mbaya kwa kukaa karibu naye.

فوائد الحديث

Inaruhusiwa kutumia mifano ili kusogeza maana karibu kwa msikilizaji.

Himizo na hamasisho kwa watu kuwa pamoja na watu watiifu na waadilifu, na kujiepusha na watu waovu na wenye maadili mabaya.

التصنيفات

Hali zawatu wema., Kuyasema vibaya Maasi.