Kuamini mikosi ni shirki, Kuamini mikosi ni shirki, Kuamini mikosi ni shirki, alisema hivyo mara tatu", Na hakuna yeyote miongoni mwetu isipokuwa ana chembe ya hilo, isipokuwa Mwenyezi Mungu huliondoa kwa kumtegemea

Kuamini mikosi ni shirki, Kuamini mikosi ni shirki, Kuamini mikosi ni shirki, alisema hivyo mara tatu", Na hakuna yeyote miongoni mwetu isipokuwa ana chembe ya hilo, isipokuwa Mwenyezi Mungu huliondoa kwa kumtegemea

Kutoka kwa Abdallah bin Masoud -Radhi za Allah ziwe juu yake- kutoka kwa Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- amesema: "Kuamini mikosi ni shirki, Kuamini mikosi ni shirki, Kuamini mikosi ni shirki, alisema hivyo mara tatu", Na hakuna yeyote miongoni mwetu isipokuwa ana chembe ya hilo, isipokuwa Mwenyezi Mungu huliondoa kwa kumtegemea.

[Sahihi] [Imepokelewa na Ibnu Maajah]

الشرح

Ametahadharisha Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- kutokana na imani ya mikosi: Nayo ni kuamini mikosi ya chochote chenye kusikika au chenye kuonekana, kama ndege au wanyama au walemavu au namba au siku au kinginecho, Na bila shaka ametaja ndege kwa sababu ndio ilikuwa maarufu kipindi cha zama za ujinga, na asili yake ni kumuachia ndege aruke katika jambo kama safari au biashara au kinginecho, akiruka pande wa kulia anajipa bishara na anatekeleza anachotaka kukifanya, na akirukia upande wa kushoto, anaamini ni mkosi na anaacha kufanya alichotaka kukifanya. Na akaeleza kuwa kitendo hicho ni ushirikina, na mikosi imekuwa ni ushirikina kwa sababu hakuna aletaye kheri ila Mwenyezi Mungu, na wala hazuii shari ila Mwenyezi Mungu yeye pekee asiye na mshirika. Na ametaja bin Masoud radhi za Allah ziwe juu yake kuwa inaweza kuingia katika moyo wa muislamu kiasi kidogo cha imani ya mkosi, lakini anatakiwa akizuie kwa kumtegemea Mwenyezi Mungu, ikiwa ni pamoja na kufanya sababu.

فوائد الحديث

Mikosi ni ushirikina; kwa sababu ndani yake kuna kuufungamanisha moyo kwa asiyekuwa Mwenyezi Mungu.

Umuhimu wa kurudia mambo muhimu, ili yahifadhike na yakite ndani ya moyo.

Mikosi huondolewa kwa kutegemea kwa Allah Mtukufu.

Amri ya kutegemea kwa Allah pekee na moyo kufungamana naye Mtukufu.

التصنيفات

Ushirikina., Ushirikina., Fadhila za matendo ya moyoni., Fadhila za matendo ya moyoni.