إعدادات العرض
Hivi yule aliyemfanya atembee kwa miguu miwili hawezi kumfanya atembee kwa uso wake siku ya Kiyama?
Hivi yule aliyemfanya atembee kwa miguu miwili hawezi kumfanya atembee kwa uso wake siku ya Kiyama?
Imepokelewa kutoka kwa Qatadah -Mwenyezi Mungu amrehemu amesema: Alitusimulia Anas Bin Maalik -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- kuwa Mtu mmoja alisema: Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu vipi kafiri atafufuliwa akitembea kwa uso wake? Akasema: "Hivi yule aliyemfanya atembee kwa miguu miwili hawezi kumfanya atembee kwa uso wake siku ya Kiyama?" Akasema Qatadah: Kwa nini asiweze, ninaapa kwa utukufu wa Mola wetu anaweza kufanya hivyo.
[Sahihi] [Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim]
الترجمة
عربي English မြန်မာ Svenska cs ગુજરાતી አማርኛ Yorùbá Nederlands اردو Español Bahasa Indonesia ئۇيغۇرچە বাংলা Türkçe Bosanski සිංහල हिन्दी Tiếng Việt Hausa മലയാളം తెలుగు ไทย پښتو অসমীয়া Shqip دری el bg ff it kn Кыргызча Lietuvių mg ro rw Soomaali Српски тоҷикӣ uz नेपालीالشرح
Aliulizwa Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- vipi atafufuliwa Kafiri akitembea kwa uso wake siku ya Kiyama? Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake-akasema: Hivi Mwenyezi Mungu aliyemfanya atembee kwa miguu miwili hapa Duniani hawezi kumfanya atembee kwa uso wake siku ya Kiyama?! Mwenyezi Mungu ni muweza wa kila kitu.فوائد الحديث
Udhalili utampata Kafiri siku ya Kiyama na atatembea kwa uso wake.