Hakika kilicho kati ya mtu na ushirikina na ukafiri ni kuacha swala

Hakika kilicho kati ya mtu na ushirikina na ukafiri ni kuacha swala

Imepokewa kutoka kwa Jabiri -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- amesema: Nilimsikia Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- akisema: "Hakika kilicho kati ya mtu na ushirikina na ukafiri ni kuacha swala".

[Sahihi] [Imepokelewa na Imamu Muslim]

الشرح

Anatahadharisha Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- kuacha swala ya faradhi, na akaeleza kuwa kati ya mtu na baina ya kuingia katika shirki na ukafiri ni kuacha swala, swala ni nguzo ya pili katika nguzo za Uislamu, na jambo lake ni kubwa katika Uislamu, atakayeiacha kwa kupinga uwajibu wake amekufuru kwa makubaliano ya waislamu, na akiiacha moja kwa moja kwa uzembe na uvivu pia ni kafiri, na yamenukuliwa makubaliano ya Masahaba juu ya hilo, na ikiwa anaiacha baadhi ya wakati na wakati mwingine anaswali, basi anajitia katika makemeo haya makubwa.

فوائد الحديث

Umuhimu wa swala na kuihifadhi, kwani ndio inayotenganisha kati ya ukafiri na imani.

Tahadhari kubwa kwa atakayeacha swala na akaitelekeza.

التصنيفات

Vichenguzi vya uislamu., Kufuru, Wajibu wa Swala na Hukumu ya Mwenye kuiwacha.