Alichinja Mtume rehema na amani ziwe juu yake kondoo wawili wazuri weupe wenye pembe, aliwachinja kwa mkono wake, akasema, Bismillahi Allaahu Akbar, na akaweka mguu wake ubavuni mwao

Alichinja Mtume rehema na amani ziwe juu yake kondoo wawili wazuri weupe wenye pembe, aliwachinja kwa mkono wake, akasema, Bismillahi Allaahu Akbar, na akaweka mguu wake ubavuni mwao

Imepokelewa kutoka kwa Anas -radhi za Mwenyezi Mungu ziwe ju yake- amesema: Alichinja Mtume rehema na amani ziwe juu yake kondoo wawili wazuri weupe wenye pembe, aliwachinja kwa mkono wake, akasema, Bismillahi Allaahu Akbar, na akaweka mguu wake ubavuni mwao.

[Sahihi] [Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim]

الشرح

Ameeleza Anasi radhi za Allah ziwe juu yake kuwa Mtume rehema na amani ziwe juu yake alichinja kwa mkono wake siku ya Idil Adh-haa kondoo wawili madume wenye mapembe, weupe wenye mchanganyiko na weusi, na akasema: Bismillaahi wallaahu Akbaru, na akaweka mguu wake katika shingo zao.

فوائد الحديث

Sheria ya kuchinja siku ya Idi kubwa (Adh-ha), na waislamu wote wamekubaliana hilo.

Kilichobora zaidi ni kuwa kichinjwa kiwe cha aina hii aliyochinja Mtume rehema na amani ziwe juu yake; kwa muonekano wake mzuri lakini pia mafuta yake na nyama yake nzuri.

Amesema Imam Nawawi: Hapa kuna sunna ya mtu asimamie mwenyewe kuchinja kichinjwa chake cha udhuhia, na wala asimuwakilishe yeyote ila kwa udhuru, na hapo pia ni sunna ashuhudie kichinjwa chake, na ikiwa atamuweka muislamu kwa niaba yake itafaa kwa itifaki ya wanachuoni.

Amesema bin Hajari: Na hapa kuna sunna ya kutoa takbira (Allaahu Akbaru) pamoja na kumtaja Mwenyezi Mungu (Bismillaah) wakati wa kuchinja, na kuweka mguu katika weupe wa shingo wa kulia wa mnyama, na wamekubaliana wanachuoni kuwa ubavu wake unakuwa upande wa kushoto ataweka mguu wake wa kulia ili iwe rahisi kumchinja wakati wa kuchukua kisu kwa mkono wa kulia na kukamata kichwa chake kwa mkono wake wa kulia

Ni sunna kichinjwa cha udh-hiya kiwe na pembe na inafaa pia kwa kinginecho.

التصنيفات

Uchinjaji., Vichinjwa.