“Mwenyezi Mungu, Aliyetakasika na Kutukuka, atawaambia watu wa Peponi: Enyi watu wa Peponi? Watasema: Labeka tumekuitikia na umetukuka, atasema: Je, mmeridhika? Watasema: Tuna nini mpaka tusiridhike hali yakuwa umetupa mambo ambayo hujampa yeyote katika viumbe wako?

“Mwenyezi Mungu, Aliyetakasika na Kutukuka, atawaambia watu wa Peponi: Enyi watu wa Peponi? Watasema: Labeka tumekuitikia na umetukuka, atasema: Je, mmeridhika? Watasema: Tuna nini mpaka tusiridhike hali yakuwa umetupa mambo ambayo hujampa yeyote katika viumbe wako?

Imepokelewa kutoka kwa Saidi Al-Khuduriy -radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- amesema: Amesema Mtume -rehema na amani ziwe juu yake-: “Mwenyezi Mungu, Aliyetakasika na Kutukuka, atawaambia watu wa Peponi: Enyi watu wa Peponi? Watasema: Labeka tumekuitikia na umetukuka, atasema: Je, mmeridhika? Watasema: Tuna nini mpaka tusiridhike hali yakuwa umetupa mambo ambayo hujampa yeyote katika viumbe wako? Atasema: Mimi nitakupeni kilicho bora zaidi kuliko hilo, Watasema: Ewe Mola Mlezi, ni kitu gani kilicho bora kuliko hili? Atasema: Ninawapeni radhi zangu, wala sitowachukia baada yake milele".

[Sahihi] [Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim]

الشرح

Ameeleza Mtume rehema na amani ziwe juu yake kuwa Mwenyezi Mungu Mtukufu atawaambia watu wa Peponi wakiwa humo: Enyi watu wa Peponi, nao watamjibu kwa kusema: Labeka, tumekuitikia Mola wetu Mlezi! na utukufu ni wako, Atasema kuwaambia: Je! mmeridhika? Watasema: Ndiyo, tumeridhika; Kwa nini tusiridhike wakati umetupa ambacho hukumpa kiumbe wako yeyote! Atasema Mtukufu: Je, nisikupeni kilicho bora kuliko hicho? Watasema: Ewe Mola Mlezi, na ni kitu gani kilicho bora kuliko hicho? Atasema: Ninakuteremshieni juu yenu radhi zangu daima; na sitokukasirikieni baada yake milele.

فوائد الحديث

Mazungumzo ya Mwenyezi Mungu Mtukufu pamoja na watu wa peponi.

Habari njema kutoka kwa Mwenyezi Mungu kwa watu wa peponi ya kuwaridhia, na kuwateremshia radhi juu yao na kutochukia tena milele.

Kila mtu Peponi ataridhika na hali yake licha ya kutofautiana viwango vyao na kupishana daraja zao; Kwa sababu wote walijibu kwa neno moja, ambalo ni: "Umetupa kile ambacho hukumpa yeyote katika viumbe vyako."

التصنيفات

Kumpwekesha Mwenyezi Mungu katika majina yake na sifa zake., Sifa za pepo na moto.