Amesimulia kuwa mtu mmoja alikula chakula kwa Mtume Rehema na amani ziwe juu yake kwa mkono wake wa kushoto, akasema: "Kula kwa mkono wako wa kulia", Akasema: Siwezi, akasema: "Kamwe, hutoweza!",

Amesimulia kuwa mtu mmoja alikula chakula kwa Mtume Rehema na amani ziwe juu yake kwa mkono wake wa kushoto, akasema: "Kula kwa mkono wako wa kulia", Akasema: Siwezi, akasema: "Kamwe, hutoweza!",

Kutoka kwa Salama bin Al Ak'wa'i -Radhi za Allah ziwe juu yake. Amesimulia kuwa mtu mmoja alikula chakula kwa Mtume Rehema na amani ziwe juu yake kwa mkono wake wa kushoto, akasema: "Kula kwa mkono wako wa kulia", Akasema: Siwezi, akasema: "Kamwe, hutoweza!", Hakuna kilichomzuia ila ni kiburi, akasema: hakuweza tena kuunyanyua kwenda kinywani kwake.

[Sahihi] [Imepokelewa na Imamu Muslim]

الشرح

Alimuona Mtume Rehema na amani ziwe juu yake mtu mmoja akila kwa mkono wake wa kushoto, akamuamrisha ale kwa mkono wake wa kulia, Yule bwana akamjibu kwa kiburi na kwa kuongopa kuwa hawezi! Mtume Rehema na amani ziwe juu yake akamuombea dua mbaya azuiliwe kula kwa mkono wa kulia, Mwenyezi Mungu akajibu dua ya Nabii wake, kwa kupooza mkono wake wa kulia, hakuweza kuunyanyua kwenda kinywani kwake baada ya hapo kwa chakula au kinywaji.

فوائد الحديث

Uwajibu wa kula kwa mkono wa kulia, na uharamu wa kula kwa mkono wa kushoto.

Kiburi katika kutekeleza hukumu za sheria mwenye kufanya hivyo anastahiki adhabu.

Ukarimu wa Mwenyezi Mungu kwa Nabii wake Muhammadi Rehema na amani ziwe juu yake kwa kujibu maombi yake.

Sheria ya kuamrisha mema na kukataza maovu kwa kila hali hata wakati wa chakula.

التصنيفات

Adabu ya kula na kunywa.