Kutoka kwa Abdillah bin Mas'udi -radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- Amesema: Amesema Mtume -rehema na amani ziwe juu yake-: "Shikamaneni na ukweli, kwani ukweli hupelekea katika wema, na hakika wema hupelekea katika pepo

Kutoka kwa Abdillah bin Mas'udi -radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- Amesema: Amesema Mtume -rehema na amani ziwe juu yake-: "Shikamaneni na ukweli, kwani ukweli hupelekea katika wema, na hakika wema hupelekea katika pepo

Kutoka kwa Abdallah bin Masoud -radhi za Allah ziwe juu yake- amesema: Amesema Mtume -rehema na amani ziwe juu yake-: Kutoka kwa Abdillah bin Mas'udi -radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- Amesema: Amesema Mtume -rehema na amani ziwe juu yake-: "Shikamaneni na ukweli, kwani ukweli hupelekea katika wema, na hakika wema hupelekea katika pepo, na hatoacha mtu kuwa mkweli na akishughulika na ukweli mpaka ataandikwa kwa Mwenyezi Mungu kuwa ni mkweli, na tahadharini na uongo, kwani uongo unapelekea katika uovu, na hakika uovu hupelekea katika moto, na hatoacha mtu kuendelea kuwa muongo, na akishughulika na uongo mpaka ataandikwa mbele ya Mwenyezi Mungu kuwa ni muongo".

[Sahihi] [Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim]

الشرح

Mtume rehema na amani ziwe juu yake ameamrisha ukweli, na akasema kuwa kushikamana nao kunapelekea katika matendo mema ya kudumu, na mwenye kushikamana na kufanya wema humpeleka mtendaji wake Peponi, na ukweli wake unapoendelea mara kwa mara kwa siri na hadharani, basi hustahiki jina la mkweli; nayo ni sifa ya hali ya juu zaidi ya ukweli. Kisha Mtume rehema na amani ziwe juu yake akaonya dhidi ya kusema uongo na kusema maneno ya batili; Kwa sababu inawachochea watu kuacha uadilifu, na kufanya maovu, ufisadi, na dhambi, kisha inawapeleka Motoni, na anapoendelea kukithirisha kusema uongo basi mpaka huandikwa kwa Mwenyezi Mungu kuwa ni miongoni mwa waongo.

فوائد الحديث

Ukweli ni tabia adhimu ambayo hupatikana kupitia juhudi, kwa sababu mtu anapoendelea kuwa mkweli na kuutafuta ukweli, mpaka ukweli unakuwa ni kama tabia yake ya asili, basi huandikwa mbele ya Mwenyezi Mungu kuwa ni miongoni mwa wa watu wakweli na wema.

Uongo ni tabia ya kulaumiwa ambayo mhusika huipata kupitia mazoea ya muda mrefu katika maneno na matendo, mpaka inakuwa ni tabia na silika yake, kisha anaandikwa mbele ya Mwenyezi Mungu kuwa ni katika waongo.

Ukweli unahusu ukweli wa ulimi, ambao ni kinyume cha uongo, na ukweli katika nia, ambao ni ikhlasi, na ukweli katika kusuluhisha vyema nia yake, na ukweli katika vitendo, na kwa uchache zaidi ni siri yake na dhahiri yake viwe sawa, na ukweli katika matukio kama kusema ukweli wakati wa hofu na raha, na mengineyo, hivyo yeyote atakayesifika na sifa hizo basi atakuwa ni mkweli mno, au akasifika na baadhi yake atakuwa mkweli pia.

التصنيفات

Tabia njema.