Atakapompenda mtu ndugu yake basi na amueleze kuwa anampenda

Atakapompenda mtu ndugu yake basi na amueleze kuwa anampenda

Imepokelewa Kutoka kwa Mikidadi bin Ma'di Yakrib -Radhi za Allah ziwe juu yake- Kutoka kwa Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake-: "Atakapompenda mtu ndugu yake basi na amueleze kuwa anampenda".

[Sahihi]

الشرح

Anabainisha Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- moja ya sababu ambazo hutia nguvu mahusiano kati ya waumini na hueneza mapenzi baina yao, nako ni kuwa mtu atakapompenda ndugu yake basi na amueleze kuwa anampenda.

فوائد الحديث

Ubora wa mapenzi ya dhati yanayokuwa kwa ajili ya Mwenyezi Mungu Mtukufu, si kwa ajili ya masilahi ya kidunia.

Inapendeza na ni sunna kumueleza anayependwa kwa ajili ya Allah, ili kuongeza mapenzi na kuzoeana.

Kuenea kwa mapenzi baina ya waumini hutia nguvu udugu wa kiimani na huhifadhi jamii kuto pasuka na kufarakana.

التصنيفات

Tabia njema., Adabu ya mazungumzo na kunyamaza.