Mwenye kutakiwa kheri na Allah humpa ufahamu katika dini

Mwenye kutakiwa kheri na Allah humpa ufahamu katika dini

Imepokewa kutoka kwa Muawiya -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- amesema: Nilimsikia Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- akisema: "Mwenye kutakiwa kheri na Allah humpa ufahamu katika dini, mimi ni mgawaji tu, na Allah ndiye anayetoa, na umma huu utaendelea kusimama katika amri ya Mwenyezi Mungu, hatowadhuru mwenye kuwapinga, mpaka ije amri ya Mwenyezi Mungu".

[Sahihi] [Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim]

الشرح

Anaeleza Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- yakuwa mwenye kutakiwa kheri na Mwenyezi Mungu basi humruzuku ufahamu katika dini yake Mwenyezi Mungu Mtukufu, nakuwa Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- ni mgawaji na msambazaji wa yale aliyopewa na Allah Mtukufu katika riziki na elimu na mengineyo, nakuwa mtoaji halisia ni Allah, na ama asiyekuwa yeye hao ni sababu tu hawawezi kunufaisha ila kwa idhini ya Mwenyezi Mungu, nakuwa umma huu utaendelea kusimama katika amri ya Mwenyezi Mungu, hatowadhuru mwenye kuwapinga, mpaka Kiyama kisimame.

فوائد الحديث

Utukufu na fadhila za elimu ya kisheria na kujifunza kwake na kuihimiza.

Kuisimamia haki ni lazima kuwepo katika umma huu, likiwacha kusimamia kundi fulani linasimama kundi jingine.

Kuisoma dini ni katika matashi ya Allah Mtukufu kumtakia kheri mja wake.

Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- anatoa kwa amri ya Mwenyezi Mungu na matashi yake, na yeye hamiliki chochote.

التصنيفات

Ubora wa Elimu., Ubora wa Elimu.