Msitengeze mabustani, mkajakuipenda sana dunia

Msitengeze mabustani, mkajakuipenda sana dunia

Kutoka kwa Abdallah bin Masoud -radhi za Allah ziwe juu yake- amesema: Amesema Mtume -rehema na amani ziwe juu yake-: "Msitengeze mabustani, mkajakuipenda sana dunia".

[Ni nzuri kwa sababu ya hadithi nyingine]

الشرح

Amekataza Mtume rehema na amani ziwe juu yake kujitengenezea makonde na mabustani na mashamba; kwa sababu hilo ni katika sababu za kuipenda sana dunia na kubweteka nayo na kuisahau Akhera.

فوائد الحديث

Katazo la kukithirisha sana hadhi za kidunia kwa sababu hupelekea kuiacha Akhera.

Katika hadithi hakuna katazo la kutengeneza yale yanayopelekea maisha, bali katazo ni kuzama katika dunia na kuisahau Akhera.

Amesema Sanadi: Na makusudio yake: Nikuwa msizame katika kutengeneza mabustani, mkapumbazika nayo na mkajisahau kumtaja Mwenyezi Mungu.

التصنيفات

Mambo mazuri na Adabu- Heshima., Kuyasema vibaya mapenzi ya kuipenda dunia.