Yakwamba Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- Alikuwa akinyanyua mikono yake usawa wa mabega yake anapofungua swala,

Yakwamba Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- Alikuwa akinyanyua mikono yake usawa wa mabega yake anapofungua swala,

Na kutoka kwa Ibn Omari Radhi za Allah ziwe juu yake na baba yake: Yakwamba Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- Alikuwa akinyanyua mikono yake usawa wa mabega yake anapofungua swala, na anapotoa takbira ya kurukuu, na anaponyanyua kichwa chake kutoka katika rukuu anainyanyua pia, na akasema: "Sami'a llaahu liman hamidahu" Yaani: Amemsikia Mwenyezi Mungu yule aliyemuhimidi, "Rabbanaa walakal hamdu" Mola wetu Mlezi na sifa njema ni zako, na alikuwa hafanyi hivyo katika sijida.

[Sahihi] [Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim]

الشرح

Mtume, rehema na amani ziwe juu yake alikuwa akinyanyua mikono yake katika sehemu tatu wakati wa kuswali, usawa wa mabega ni: Pale panapounga kati ya mfupa wa bega na mkono. Sehemu ya kwanza: Anapofungua swala wakati wa takbira ya kuhirimia swala. Sehemu ya pili: Anapotoa takbira kwa ajili ya rukuu. Sehemu ya tatu: Anaponyanyua kichwa chake kutoka katika rukuu, na akasema: Sami'allahu liman hamidah, Rabbanaa walakal hamdu. Amemsikia Mwenyezi Mungu mwenye kumhimidi, Mola wetu Mlezi, na sifa njema ni zako. Na alikuwa hanyanyui mikono yake wakati wa kuanza kusujudu, wala wakati wa kunyanyua kutoka katika sijida.

فوائد الحديث

Katika hekima za kunyanyua mikono ndani ya swala, ni pambo la swala, na ni kumtukuza Mwenyezi Mungu Mtukufu.

Imethibiti kutoka kwake rehema na amani ziwe juu yake, kuwa alinyanyua mikono yake katika nafasi ya nne, kama ilivyokuja katika riwaya ya Abuu Humaid Al-Sa'idi kwa Abuu Daudi na wengineo, ambayo ni wakati wa kusimama kutoka tashahudi ya kwanza. katika swala ya rakaa tatu na nne.

Imethibiti vile vile kutoka kwake rehema na amani zimshukie, pia alikuwa akinyanyua mikono yake usawa wa masikio yake bila ya kuyagusa, kama ilivyo katika riwaya ya Maliki bin Al-Huwairith katika Sahihi mbili: “Yakwamba Mtume wa Mwenyezi Mungu rehema na amani zimshukie, alikuwa akinyanyua mikono yake mpaka inalingana na masikio yake.”

Na kukusanya kati ya kusema: "Sami'allaahu liman hamidah, na kusema: "Rabbanaa walakal hamdu, hii ni maalumu kwa Imamu na anayeswali peke yake, ama maamuma yeye atasema: Rabbanaa walakal hamdu, pekee.

Kusema: Rabbanaa walakal hamdu “Mola wetu Mlezi na sifa njema ni zako” baada ya kurukuu ni sahihi kutoka kwa Mtume rehema na amani ziwe juu yake, kuna namna nne, na hii ni mojawapo, na ni bora kwa mtu afuatilie namna hizi zote, ili wakati mwingine analeta hii, na wakati mwingine analeta hii.

التصنيفات

Sifa za Swala.