Hakika ninachokiogopea zaidi juu yenu ni shirki ndogo" Wakasema: Ni ipi shirki ndogo ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu? Akasema: "Ni riyaa (kujionyesha)

Hakika ninachokiogopea zaidi juu yenu ni shirki ndogo" Wakasema: Ni ipi shirki ndogo ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu? Akasema: "Ni riyaa (kujionyesha)

Imepokelewa kutoka kwa Mahmud bin Labid -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- Yakuwa Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- amesema: "Hakika ninachokiogopea zaidi juu yenu ni shirki ndogo" Wakasema: Ni ipi shirki ndogo ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu? Akasema: "Ni riyaa (kujionyesha), atasema Mwenyezi Mungu Mtukufu siku ya Kiyama kuwaambia, pindi watu wote watakapolipwa kwa matendo yao: 'Nendeni kwa wale mliokuwa mkijionyesha kwao duniani, mtazame je mtapata kwao malipo?".

[Ni nzuri] [Imepokelewa na Ahmad]

الشرح

Anaeleza Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- yakuwa jambo kubwa zaidi analoliogopea juu ya umma wake: Ni shirki ndogo nayo; ni mtu kufanya kwa ajili ya watu. Kisha akaeleza kuhusu adhabu ya wenye kujionyesha siku ya Kiyama kwa kuambiwa: Nendeni kwa wale mliokuwa mkifanya kwa ajili yao, mkatazame je wanamiliki malipo na thawabu za kukupeni kwa amali hiyo?!.

فوائد الحديث

Ulazima wa kutakasa matendo kwa ajili ya Mwenyezi Mungu Mtukufu, na kutahadhari na riyaa.

Huruma yake kubwa Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- juu ya umma wake na pupa yake ya kutaka kuwaongoza na kuwapa kwake nasaha.

Ikiwa hii ndio hofu yake Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- akizungumza na Masahaba ambao ndio watukufu kwa watu wema, basi hofu kwa wale wataokuja baada yao ni kubwa zaidi.

التصنيفات

Ushirikina., Huruma zake Mtume Rehma na za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake amani: