Mwenye kuisoma Qur'ani kwa sauti ya wazi ni kama mwenye kutoa sadaka hadharani, na mwenye kuisoma Qur'ani kwa siri ni kama mwenye kuficha sadaka

Mwenye kuisoma Qur'ani kwa sauti ya wazi ni kama mwenye kutoa sadaka hadharani, na mwenye kuisoma Qur'ani kwa siri ni kama mwenye kuficha sadaka

Imepokelewa kutoka kwa Uqbah Bin Aamir Al-juhaniy-Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake-amesema: Amesema Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake: "Mwenye kuisoma Qur'ani kwa sauti ya wazi ni kama mwenye kutoa sadaka hadharani, na mwenye kuisoma Qur'ani kwa siri ni kama mwenye kuficha sadaka."

[Sahihi] [Imepokelewa na Abuu Daud]

الشرح

Ameweka wazi Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- kuwa mwenye kuweka wazi kusoma Qur'ani ni sawa na mwenye kuweka wazi anapotoa sadaka, na mwenye kuficha kisomo cha Qur'ani ni sawa na mwenye kuificha sadaka.

فوائد الحديث

Kuficha usomaji wa Qur'ani ni bora, kama ilivyo kuficha sadaka ni bora zaidi, kwa kuwa kufanya hivyo ni katika utakasifu wa nia na kujiweka mbali na kujionesha na kujisikia, isipokuwa itakapohitajika, na maslahi ya kuisoma kwa wazi ni katika kuifundisha.

التصنيفات

Ubora wa Qur'an tukufu., Ubora wa Qur'an tukufu., Fadhila za matendo ya moyoni., Fadhila za matendo ya moyoni., Adabu za usomaji wa Qur'an., Adabu za usomaji wa Qur'an.