Hakika utakuja kutokea uchoyo na kujipendelea baada yangu na mambo msiyoyajua (uzushi)" Wakasema: Ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu unatuamrisha nini? Akasema: "Mtekeleze haki ya wajibu kwenu, na mumuombe Allah haki yenu

Hakika utakuja kutokea uchoyo na kujipendelea baada yangu na mambo msiyoyajua (uzushi)" Wakasema: Ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu unatuamrisha nini? Akasema: "Mtekeleze haki ya wajibu kwenu, na mumuombe Allah haki yenu

Imepokelewa kutoka kwa Bin Masoud -Radhi za Allah ziwe juu yake- kutoka kwa Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- amesema: "Hakika utakuja kutokea uchoyo na kujipendelea baada yangu na mambo msiyoyajua (uzushi)" Wakasema: Ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu unatuamrisha nini? Akasema: "Mtekeleze haki ya wajibu kwenu, na mumuombe Allah haki yenu".

[Sahihi] [Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim]

الشرح

Alieleza Mtume Rehema na amani ziwe juu yake yakuwa waislamu watatawaliwa na viongozi watakaohodhi na kujipendelea mali za waislamu na mambo mengine mengi yasiyokuwa mali, watazitumia kama watakavyo, na watawanyima waislamu haki yao katika mali hizo. Na watakuwa na mambo ndani ya dini mtakayoyakataa kuwa si katika dini. Masahaba Radhi za Allah ziwe juu yao wakauliza: Ni nini watafanya katika hali kama hiyo? Akawaeleza Rehema na amani ziwe juu yake kuwa kusikuzuieni kule kuhodhi kwao mali na kujipendelea kwao, nanyi mkaacha kufanya wajibu wenu kwao, ikiwemo usikivu na utii, bali kuweni na subira na mtii msiwaletee upinzani katika madaraka, na haki yenu iombeni kutoka kwa Allah, na awarekebishe na azuie shari zao na dhulma zao.

فوائد الحديث

Hadithi hii ni katika dalili za utume wake Rehema na amani ziwe juu yake, kiasi ambacho alieleza mambo yatakayotokea ndani ya Umma wake na yakatokea kama alivyoeleza.

Inafaa kumueleza mtahiniwa yale yatakayomsibu katika mitihani; ili aitulize nafsi yake, mtihani ukimfika atakuwa na subira na atataraji malipo toka kwa Allah.

Kushikamana na Qur'ani na Sunna ni sababu ya kutoka katika fitina na hitilafu.

Himizo la kuwa wasikivu na watiifu kwa viongozi katika mema, na kutojitoa katika utiifu, hata kama zitatokea kwao dhulma.

Kutumia hekima na kufuata mafundisho ya Mtume wakati wa fitina.

Ni jukumu la kila mtu kutimiza haki ya msingi inayomlazimu hata kama itatokea kadhulumiwa.

Hadithi inaashiria kanuni ya msingi ambayo ni: Mtu kuchagua moja kati ya shari mbili au madhara yenye nafuu.

التصنيفات

Uwajibu wa Kiongozi.