Acha linalokutia shaka fanya lisilokutia shaka, kwani ukweli ni utulivu, na bila shaka uongo ni shaka

Acha linalokutia shaka fanya lisilokutia shaka, kwani ukweli ni utulivu, na bila shaka uongo ni shaka

Kutoka kwa Abul Hauraai Assa'di amesema: Nilisema kumwambia Hassan bin Ally radhi za Allah ziwe juu yao: Ulihifadhi nini kutoka kwa Mtume rehema na amani ziwe juu yake? Akasema: Nilihifadhi kutoka kwa Mtume rehema na amani ziwe juu yake? "Acha linalokutia shaka fanya lisilokutia shaka, kwani ukweli ni utulivu, na bila shaka uongo ni shaka"

[Sahihi] [Imepokelewa na Imamu Tirmidhiy - Imepokelewa na An-Nasaaiy - Imepokelewa na Ahmad - Imepokelewa na Addaaramy]

الشرح

Aliamrisha Mtume rehema na amani ziwe juu yake kuacha kile ulicho na shaka nacho katika maneno na matendo nakuwa jambo hilo limekatazwa toka mwanzo, je jambo hili ni halali au ni haramu, afanye asilo na shaka nalo katika yale ambayo anaamini kuwa ni mazuri na ni halali, kwa sababu moyo unatulizana na unatulia katika hilo, na hakuna shaka ndani yake inayotia msongo na taharuki.

فوائد الحديث

Muislamu anatakiwa kujenga mambo yake juu ya yakini na kuacha yenye kutia shaka ndani yake, na awe na utambuzi katika dini yake.

Katazo la kutumbukia katika matamanio mabaya.

Ukitaka utulivu na raha achana na mambo yanayokutia shaka na kuyatupilia mbali.

Huruma ya Mwenyezi Mungu kwa waja wake, pale alipowaamrisha katika mambo ambayo ndani yake kuna raha ya moyo, na akawakataza katika yale yanayotia msongo na utata.

التصنيفات

Kukinzana na Kufanya kuwa ni sahihi.