Atakapoingia mmoja wenu msikitini basi asali rakaa mbili kabla hajakaa

Atakapoingia mmoja wenu msikitini basi asali rakaa mbili kabla hajakaa

Kutoka kwa Abuu Qatada As-sulami Radhi za Allah ziwe juu yake- hakika Mtume Rehema na amani za Allah ziwe juu yake alisema: "Atakapoingia mmoja wenu msikitini basi asali rakaa mbili kabla hajakaa".

[Sahihi] [Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim]

الشرح

Amemhimiza Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- mwenye kuja msikitini na akaingia katika wakati wowote, na kwa lengo lolote, asali rakaa mbili kabla hajakaa, nazo ni rakaa mbili za salamu ya msikiti.

فوائد الحديث

Sunna ya swala ya rakaa mbili kwa ajili ya salamu ya msikiti kabla ya kukaa.

Amri hii ni kwa atakayetaka kukaa, atakayeingia msikitini na akatoka kabla ya kukaa, amri hii haimuhusu.

Atakapoingia mwenye kuswali na watu wakiwa ndani ya swala, akaingia nao, basi hilo litamtosheleza na rakaa mbili.

التصنيفات

Swala ya Kujikurubisha kwa Mwenyezi Mungu., Hukumu za Misikiti.