إعدادات العرض
Swala tano, na ijumaa mpaka ijumaa, na Ramadhani hadi Ramadhani, hufuta madhambi yaliyo kati yake, ikiwa mtu atayaepuka madhambi makubwa
Swala tano, na ijumaa mpaka ijumaa, na Ramadhani hadi Ramadhani, hufuta madhambi yaliyo kati yake, ikiwa mtu atayaepuka madhambi makubwa
Kutoka kwa Abuu Huraira -Radhi za Allah ziwe juu yake- yakwamba Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- alikuwa akisema: "Swala tano, na ijumaa mpaka ijumaa, na Ramadhani hadi Ramadhani, hufuta madhambi yaliyo kati yake, ikiwa mtu atayaepuka madhambi makubwa"
[Sahihi] [Imepokelewa na Imamu Muslim]
الترجمة
ar bn bs en es fa fr id ru tl tr ur zh hi si ku ha pt ml te my de ja ps vi as sq sv cs gu yo nl ug ta prs bg ff hu kn ky lt or ro rw tg uz ak ne mos az wo om so uk bm km rn ka mk sr el am mgالشرح
Anaeleza Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- kuwa swala tano za faradhi za usiku na mchana, na swala ya ijumaa kila wiki, na funga ya Ramadhani kila mwaka, vyote hivi hufuta madhambi madogo madogo yaliyo kati yake, kwa sharti la kuyaepuka madhambi makubwa, Ama madhambi makubwa kama zinaa na kunywa pombe haya hayafutwi isipokuwa kwa toba.فوائد الحديث
Madhambi yako madogo madogo na yako makubwa.
Kufutiwa madhambi madogo madogo kumewekwa sharti la ya kuyaepuka makubwa.
Madhambi makubwa ni yale iliyokuja adhabu ndani yake katika dunia, au yaliyotajwa kuwa na ahadi ya adhabu huko Akhera; au Makasiriko, au kukawa na kemeo ndani yake, au kulaaniwa mfanyaji wake, kama zinaa na unywaji pombe.